Friday 7 August 2015

MAHAKAMA YA MUAGA RAIS JAKAYA KIKWETE





Jaji mkuu OTHMAN CHANDE amempongeza Rais JAKAYA KIKWETE kwa hatua mbalimbali za kuimarisha na kuboresha shughuli za kimahakama na sheria na kuzingatia misingi ya utawala bora.

Akizungumza wakati wa mkutano Rais KIKWETE kuwaaga viongozi na watumishi wa mahakama Jaji CHANDE amesema anamshukuru Rais kwa kufuatilia na kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo.

Jaji Mkuu ametaja baadhi ya changamoto zilizopatiwa ufumbuzi kuwa ni pamoja na ujenzi na maboresho ya majengo ya mahakama na ujenzi wa nyumba za mahakimu na kuongeza idadi ya watendaji wa mahakama wakiwemo mahakaimu na majaji.

Aidha pia amempongeza Rais KIKWETE kwa kuweka uwiano mzuri wa uteuzi wa watendaji wa mahakama kwa kuzingatia usawa wa kijinsia ambapo hivi sasa majaji wanawake wamefikia asilimia 41 kati ya majaji wote TANZANIA.

Hafla hiyo imehudhuriwa na Majaji wa mahakama kuu majaji wafawidhi majaji wastaafu, majaji wakuu wa rufani na majaji viongozi. Waziri wa katiba na sheria, Rais wa chama cha wanasheria Tanzania, wasajili wakurugenzi na watumishi wa mahakama.
@@@@@@@@@



Wadau wa mazingira katika nchi za  Jumuiya  ya AFRIKA Mashariki wametakiwa kushirikiana ili kukabiliana na ongezeko la mmea wa GUGUMAJI ambao unatishia kutoweka kwa viumbe wa majini kwenye ziwa VICTORIA.
 
Wito huo umetolewa na Naibu Waziri wa Ushirikiamo wa AFRIKA Mashariki Dakta ABDULLA JUMA SAADALA   mwishoni mwa ziara yake ya  kutembelea kituo cha kuzalisha wadudu aina ya MBAWAKAVU ambao wanatumika kushambulia mmea wa GUGUMAJI kilichopo katika Chuo Cha Uvuvi  cha NYEGEZI mkoani MWANZA.

Naibu Waziri SAADALA amesema kuwa licha ya wadudu hao kufanikiwa kupunguza mmea wa GUGUMAJI katika ziwa victoria jitihada zaidi bado zinahitajika.



Waziri  wa  Ardhi, Nyumba  na  Maendeleo  ya  Makazi  WILIAM  LUKUVI  ametoa muda wa miezi  Mitatu kwa Halmashauri ya Jiji la MBEYA kuhakikisha  makubaliano  yanafikiwa na wakazi wa  eneo la SISITIRA  kabla ya wakazi hao kutoa maeneo yao ili kupisha  ujenzi  wa  Chuo Kikuu Cha Sayansi na Teknolojia MBEYA – MIST.
 
Waziri LUKUVI  ametoa muda huo mara  baada  ya  kutembelea  eneo  hilo la SISITIRA  ambalo kwa muda mrefu wakazi wake wamekua wakitaka walipwe  fidia  kabla  ya  kupisha  ujenzi wa Chuo Kikuu hicho.

Mara baada ya kuzungumza na wakazi wa eneo hilo,  wa
ziri  LUKUVI pamoja na mambo mengine ametaka kufanyika upya kwa tathmini ya maeneo ya wakazi hao.
@@@@@@@@@@@@@













Zoezi la ukoaji linaendelea katika bahari ya Mediteranian baada ya boti waliokuwa wakisafaria wahamiaji haramu kuzama katika pwani ya LIBYA.

Vikosi vya ukoaji vikiongozwa na jeshi la majini vya IRELAND  pamoja na ITALIA vinaendelea na kazi ya uokoaji ambapo watu 400 wameokolewa wengi wao wakiwa wanawake na watoto. Katika ajali hiyo watu  25 wamepoteza maisha.

Mmoja ya waokoaji amesema zoezi hilo limekabiliwa na changamoto kutokana kutofahamika idadi kamili ya watu waliokuwa wakisafiri katika boti hiyo.

Wakati huo huo msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani-  UNHCR ,MELISSA FLEMING amesema idadi kubwa ya wahamiaji wamekuwa wakikimbia vita na machafuko katika nchi zao

LEMING amekiri kuwa safari za wahamiaji wanaokimbilia barani ULAYA zimekuwa zikihatarisha maisha yao.
@@@@@@@@@@@










Wataalamu wa ndege kutoka nchi za UFARANSA, MALAYSIA na AUSTRALIA wamegudua kuwa bawa la ndege lililopatikana Magharibi mwa bahari ya HINDI katika visiwa vya REUNION, lilikuwa la shirika la ndege ya MALAYSIA MH 370.

Waziri mkuu wa MALYSIA NAJIB RAZAK amezungumza baada ya matokea hayo na kusema licha ya maumivu watakayopata familia za waathirika uthibitisho huo utatoa uhakika wa kile kilichotokea.

Ndugu wa familia zilizoathirika wamekuwa na mashaka kuhusu uchunguzi huo na   kudai kuwa wanahitaji miili ya wapendwa wao waweze kuwafanyia mazishi ya heshima.

Aidha  serikali ya AUSTRALIA kupitia waziri wake mkuu,TONY ABBOTT imesema ugunduzi huo umetoa mwanga katika kutatua tatizo.

Ndege ya shirika la ndege la MALYSIA MH 370 ilipotea March mwaka jana wakati ikifanya safari zake ikitokea KUALA LUMPAR kuelekea BEIJING na kuuwa  abiria woete  239 kwenye ndege hiyo.


Thursday 6 August 2015

MWENYEKITI WA CHAMA CHA CUF PROFESA IBRAHIM LIPUMBA ATANGAZA KUJIUZULU WADHIFA WAKE.





Mwenyekiti wa chama cha wananchi CUF Profesa IBRAHIM LIPUMBA leo ametangaza kujiuzulu wadhifa wake katika mkutano wake na waandishi wa habari uliofanyika jijini DSM.




Profesa LIPUMBA amesema amechukua hatua hiyo kutokana na Umoja wa Katiba ya wanananchi UKAWA unaoundwa na vyama vya NCCR MAGEUZI, CHADEMA, CUF na NLD kushindwa kusimamia makubaliano, ambapo amesema atabaki kuwa mwanachama tu katika chama hicho.




Wakati huo huo, Kaimu  Mkurugenzi wa habari uenezi na mawasiliano chama cha wananchi CUF Zanzibar  ISMAIL JUSS LADU  amesema kuwa Chama  cha Wananchi  CUF  hakiwezi kuyumba kwa kuondokewa   na aliyekuwa Mwenyekiti wake Prof. IBRAHIMU  LIPUMBA.




Akizungumza na waandishi wa habari  mjini Unguja JUSSA amesema maamuzi ya kujiuzulu Prof. IBRAHIMU LIPUMBA ni maamuzi yake binafsi ambayo wanayaheshimu na Chama kitaendelea kusonga mbele. 




Hatahivyo amesema mchango wake  alioweza kuutoa katika kipindi chake cha Uongozi , CUF itaendelea kuuenzi na kuuheshimu licha ya yeye kujiuzulu nafasi hiyo.



Akizungumzia kuhusu suala la umoja wa UKAWA ndio chanzo cha Profesa LIPUMBA  kujiuzulu, JUSSA amesema si kweli kwani maamuzi yote ya Chama yalikuwa yakifanywa chini yake na kushirikishwa vyema .




Hivi sasa Baraza Kuu la CUF limepanga kuanza kufanya vikao vyake ili kuweza kuziba pengo hilo aliloacha Profesa LIPUMBA .
































































RAIS WA ZANZIBAR DKT ALI MOHAMED SHEINAFUNGUA KITUO CHA WANAWAKE CHA UJASIRIAMALI



Rais wa ZANZIBAR Dkt. ALI MOHAMED SHEIN ametoa wito kwa wanawake nchini kuchangamkia fursa za mafunzo yanayotolewa katika kituo cha kufundisha wanawake utengenezaji wa vifaa vya umeme wa jua na ujasiriamali alichokifungua katika kijiji cha KIBOKWA, wilaya ya Kasazini ‘A’, Mkoa wa KASKAZINI UNGUJA.

Akizungumza katika ufunguzi wa kituo hicho, Dkt. SHEIN amesema kituo hicho kinatoa mafunzo kwa wanawake wote hata waliokosa fursa ya kwenda shule ikiwa ni utekelezaji wa mipango ya serikali kuwawezesha wanawake kuimarisha ujasiriamali.

Kwa upande wake, Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii,Vijana, Wanawake na Watoto Zanzibar ZAINAB OMAR MOHAMED amesema uzinduzi wa kituo hicho umefungua ukurasa mpya wa harakati za maendeleo ya wanawake.

Kituo hicho kimegharimu shilingi milioni mia moja na ishirini na nne ambapo Serikali ya Mapinduzi ZANZIBAR imetoa shilingi milioni 76 wakati shilingi milioni 48 zimetolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia wanawake.








MAHAKAMA NCHINI KUMUUAGA RAIS JAKAYA KIKWETE





Serikali ya awamu ya nne katika mahakama nchini Imesaidia kuboresha utoaji wa haki kwa wakati ,kukuza utawala bora, kulinda amani ya nchi na ukuaji  wa demokrasia.

Akizungumza katika hafla ya kumuaga aliyoandaliwa na mahakama kuu nchini, KIKWETE amesema serikali yake imefanikiwa kuongeza bajeti ya mahakama hadi kufikia bilioni 89, kuongeza watumishi wa mahakama ikiwemo majaji kwa uwiano wa jinsia na kuboresha maslahi ya watendaji jambo linalopelekea mahakama kufanya kazi kwa ufanisi.
                      
Hafla hiyo ya kumuaga Rais JAKAYA KIKWETE imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa ulinzi na usalama,  majaji wa Mahakama Kuu, wanasheria wa serikali na mawakili.















HABARI ZA AFRIKA NA ZA KIMATAIFA ZILIZOTIKISA LEO





Serikali ya CAMEROON imesema wapiganaji wa kikundi cha BOKO HARAM cha nchini NIGERIA wamewateka nyara watu 135, kaskazini mwa CAMEROON. Wapiganaji hao pia wamewaua watu wengine wanane katika eneo hilo.

Wapiganaji wa kikundi cha BOKO HARAM mara kadhaa wamekuwa wakifanya mashambulio ya kigaidi nchini NIGERIA, na katika nchi jirani na hivyo kuhatarisha usalama katika nchi hizo. Viongozi wan chi za AFRIKA Magharibi, walikubaliana kuunganisha majeshi yao ili kupambana na wapiganaji hao wa kikundi cha BOKO HARAM.

 Hata hivyo wapiganaji hao wamekuwa wakiendelea na mashambulio dhidi ya raia katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Wiki iliyopita rais MUHAMADU BUHARI, wa NIGIERIA, alikwenda nchini CAMEROON, kuomba msaada zaidi ya kijeshi ili kuwadhibiti wapiganaji hao wa kikundi cha BOKO HARAM.

Serikali ya MISRI inatarajia kupanua mfereji ya SUEZ, unaotumika kupitishia meli kubwa za kibiashara kutoka barani ULAYA kwenda katika maeneo mengine ya dunia.

MISRI imedhamiria kupanua mfereji huo, ili kuongeza idadi ya meli zinazosafiri kupitia mfereji huo na kuliongezea taifa hilo pato. Kupanuliwa kwa mfereji huo pia kutasaidia kupunguza misululu ya meli zinayosubiri kupita katika mfereji wa SUEZ.

Ujenzi wa mfereji huo unaotarajiwa kuanza leo ALHAMIS utagharimu YURO Bilioni SABA. Mfereji wa SUEZ unaoziunganisha bahari za MEDITERANIAN, mto NILE na hatimaye kuelekea kwenye yaSHAM ni kiungo kikubwa kati ya nchi za ULAYA na ASIA.

Vikosi vya ukoaji vya nchini ITALIA, vikiongozwa na jeshi la majini la IRELAND vinaendelea na zoezi la uokoaji katika bahari ya MEDITERANIAN baada ya boti iliyokuwa imebeba abiria zaidi ya 600 kuzama baharini.

Hadi sasa waokoaji wamefanikiwa kuwaokoa watu 400 wengi wao wakiwa wanawake na watoto.  Watu 25 wamethibitika kufa katika ajali hiyo iliyotokea karibu na pwani ya LIBYA na watu hao walikuwa ni wahamiaji waliokuwa wakielekea barani ULAYA.

Wokoaji wanasema, zoezi hilo linakabiliwa na changamoto kwa waokoaji kutojua idadi kamili ya watu waliokuwa wakisafiri ndani ya boti hiyo.

Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani-  UNHCR ,MELISSA FLEMING amesema idadi kubwa ya wahamiaji wamekuwa wakikimbia vita na machafuko katika nchi zao

Polisi nchini KENYA wamewaachia huru wanafunzi TISA, kati ya wanafunzi KUMI NAMMOJA waliotiwa nguvuni kwa tuhuma za kuchoma bweni katika shule ya sekondari ya wavulana, wanayosoma ya STEPH JOY.

Polisi pia wamewafungulia mashtaka ya kuhusika na vifo, wanafunzi watatu wa shule hiyo waliokamatwa mapema wiki hii. Wanafunzi watatu wa shule hiyo ya sekondrii ya STEPH JOY, walikufa baada ya bweni lao kuchomwa moto.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo alilazimika kukimbizwa hospitalini baada ya kupoteza fahamu, kutokana na mshituko wa tukio hilo. Polisi wanasema moto huo haukutokana na hitilafu ya umeme, bali uliwashwa kwa makusudi na watu.




Baadhi ya ndugu na jamaa za watu waliokufa baada ya ndege ya MALAYSIA, MH 370 kupotea katika mazingira ya kutatanisha mwaka jana, wanasema hawaamini kwamba mabaki, ya ndege hiyo yamepatikana katika bahari ya HINDI.
Watu hao, kutoka CHINA wanataka serikali ya MALAYSIA kuwapatia maelezo ya kutosha kuhusiana na ndugu zao. 

Idadi kubwa ya abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo ni raia wa CHINA na wanasema hawaamini kama bawa na ndege lililookotwa katika visiwa vya RE-UNION ni la ndege hiyo.

Waziri mkuu wa MALAYSIA, anadai kuwa mabaki kipande cha bawa hilo lililookotwa ni sehemu ya ndege hiyo iliyopotea mwaka jana, na hakupatikana hadi leo. Amesema kupatikana kwa ndege hiyo kutasaidia kubainisha kile kilichotokea kabla ya ndege hiyo kuanguka.

Zaidi ya watu 15 wamekufa na wengine 20 kujeruhiwa nchini SAUD ARABIA, baada ya mtu mmoja kujitoa mhanga ndani ya msikiti mmoja. Habari zinasema idadi kubwa ya watu wanaopendelea kuswali katika msikiti huo ni askari wa kikosi maalum cha jeshi la SAUDI ARABIA.

Tukio hilo limetoka katika jimbo la ASIR, linalopakana na nchi jirani ya YEMEN. Habari zinasema milipuko mingine miwili ilitokea ikiambatana na mlipuko huo wa mskitini.

Ingawa hadi sasa hakuna kikundi chochote kilichodai kuhusika na tukio hilo, lakini wapiganaji wa kikundi cha IS na wale wa kikundi cha HOUTHI cha nchini YEMEN wanatuhumiwa kuhusika.

Mizigo ipatao elfu mbili, iko katika uwanja wa ndege wa BARCELONA nchini HISPANIA, ikisubiri kuchukuliwa na abiria, waliyolazimika kuiacha kwenye uwanja huo wa ndege baada ya shirika moja la ndege kufuta safari zake.

Shirika hilo la ndege la HISPANIA linaushutumu uongozi wa uwanja wa ndege wa FUMACHINO, ambao ulilazimika kuufunga uwanja huo ukihofia moto uliotatiza safari za ndege. Moto ulio ulikuwa ukiwaka kwenye msitu, unaopakana na wanja wa ndege wa FUMACHINO, na hivyo kutatiza safari za ndege.

Abiria wanaomiliki mizigo hiyo wametakiwa kwenda kwenye uwanja huo wa ndege kuitambua.

TUPE MAONI YAKO