Thursday, 6 August 2015

HABARI ZA AFRIKA NA ZA KIMATAIFA ZILIZOTIKISA LEO





Serikali ya CAMEROON imesema wapiganaji wa kikundi cha BOKO HARAM cha nchini NIGERIA wamewateka nyara watu 135, kaskazini mwa CAMEROON. Wapiganaji hao pia wamewaua watu wengine wanane katika eneo hilo.

Wapiganaji wa kikundi cha BOKO HARAM mara kadhaa wamekuwa wakifanya mashambulio ya kigaidi nchini NIGERIA, na katika nchi jirani na hivyo kuhatarisha usalama katika nchi hizo. Viongozi wan chi za AFRIKA Magharibi, walikubaliana kuunganisha majeshi yao ili kupambana na wapiganaji hao wa kikundi cha BOKO HARAM.

 Hata hivyo wapiganaji hao wamekuwa wakiendelea na mashambulio dhidi ya raia katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo. Wiki iliyopita rais MUHAMADU BUHARI, wa NIGIERIA, alikwenda nchini CAMEROON, kuomba msaada zaidi ya kijeshi ili kuwadhibiti wapiganaji hao wa kikundi cha BOKO HARAM.

Serikali ya MISRI inatarajia kupanua mfereji ya SUEZ, unaotumika kupitishia meli kubwa za kibiashara kutoka barani ULAYA kwenda katika maeneo mengine ya dunia.

MISRI imedhamiria kupanua mfereji huo, ili kuongeza idadi ya meli zinazosafiri kupitia mfereji huo na kuliongezea taifa hilo pato. Kupanuliwa kwa mfereji huo pia kutasaidia kupunguza misululu ya meli zinayosubiri kupita katika mfereji wa SUEZ.

Ujenzi wa mfereji huo unaotarajiwa kuanza leo ALHAMIS utagharimu YURO Bilioni SABA. Mfereji wa SUEZ unaoziunganisha bahari za MEDITERANIAN, mto NILE na hatimaye kuelekea kwenye yaSHAM ni kiungo kikubwa kati ya nchi za ULAYA na ASIA.

Vikosi vya ukoaji vya nchini ITALIA, vikiongozwa na jeshi la majini la IRELAND vinaendelea na zoezi la uokoaji katika bahari ya MEDITERANIAN baada ya boti iliyokuwa imebeba abiria zaidi ya 600 kuzama baharini.

Hadi sasa waokoaji wamefanikiwa kuwaokoa watu 400 wengi wao wakiwa wanawake na watoto.  Watu 25 wamethibitika kufa katika ajali hiyo iliyotokea karibu na pwani ya LIBYA na watu hao walikuwa ni wahamiaji waliokuwa wakielekea barani ULAYA.

Wokoaji wanasema, zoezi hilo linakabiliwa na changamoto kwa waokoaji kutojua idadi kamili ya watu waliokuwa wakisafiri ndani ya boti hiyo.

Msemaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi duniani-  UNHCR ,MELISSA FLEMING amesema idadi kubwa ya wahamiaji wamekuwa wakikimbia vita na machafuko katika nchi zao

Polisi nchini KENYA wamewaachia huru wanafunzi TISA, kati ya wanafunzi KUMI NAMMOJA waliotiwa nguvuni kwa tuhuma za kuchoma bweni katika shule ya sekondari ya wavulana, wanayosoma ya STEPH JOY.

Polisi pia wamewafungulia mashtaka ya kuhusika na vifo, wanafunzi watatu wa shule hiyo waliokamatwa mapema wiki hii. Wanafunzi watatu wa shule hiyo ya sekondrii ya STEPH JOY, walikufa baada ya bweni lao kuchomwa moto.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo alilazimika kukimbizwa hospitalini baada ya kupoteza fahamu, kutokana na mshituko wa tukio hilo. Polisi wanasema moto huo haukutokana na hitilafu ya umeme, bali uliwashwa kwa makusudi na watu.




Baadhi ya ndugu na jamaa za watu waliokufa baada ya ndege ya MALAYSIA, MH 370 kupotea katika mazingira ya kutatanisha mwaka jana, wanasema hawaamini kwamba mabaki, ya ndege hiyo yamepatikana katika bahari ya HINDI.
Watu hao, kutoka CHINA wanataka serikali ya MALAYSIA kuwapatia maelezo ya kutosha kuhusiana na ndugu zao. 

Idadi kubwa ya abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo ni raia wa CHINA na wanasema hawaamini kama bawa na ndege lililookotwa katika visiwa vya RE-UNION ni la ndege hiyo.

Waziri mkuu wa MALAYSIA, anadai kuwa mabaki kipande cha bawa hilo lililookotwa ni sehemu ya ndege hiyo iliyopotea mwaka jana, na hakupatikana hadi leo. Amesema kupatikana kwa ndege hiyo kutasaidia kubainisha kile kilichotokea kabla ya ndege hiyo kuanguka.

Zaidi ya watu 15 wamekufa na wengine 20 kujeruhiwa nchini SAUD ARABIA, baada ya mtu mmoja kujitoa mhanga ndani ya msikiti mmoja. Habari zinasema idadi kubwa ya watu wanaopendelea kuswali katika msikiti huo ni askari wa kikosi maalum cha jeshi la SAUDI ARABIA.

Tukio hilo limetoka katika jimbo la ASIR, linalopakana na nchi jirani ya YEMEN. Habari zinasema milipuko mingine miwili ilitokea ikiambatana na mlipuko huo wa mskitini.

Ingawa hadi sasa hakuna kikundi chochote kilichodai kuhusika na tukio hilo, lakini wapiganaji wa kikundi cha IS na wale wa kikundi cha HOUTHI cha nchini YEMEN wanatuhumiwa kuhusika.

Mizigo ipatao elfu mbili, iko katika uwanja wa ndege wa BARCELONA nchini HISPANIA, ikisubiri kuchukuliwa na abiria, waliyolazimika kuiacha kwenye uwanja huo wa ndege baada ya shirika moja la ndege kufuta safari zake.

Shirika hilo la ndege la HISPANIA linaushutumu uongozi wa uwanja wa ndege wa FUMACHINO, ambao ulilazimika kuufunga uwanja huo ukihofia moto uliotatiza safari za ndege. Moto ulio ulikuwa ukiwaka kwenye msitu, unaopakana na wanja wa ndege wa FUMACHINO, na hivyo kutatiza safari za ndege.

Abiria wanaomiliki mizigo hiyo wametakiwa kwenda kwenye uwanja huo wa ndege kuitambua.

Wednesday, 5 August 2015

CATHY AKIPONGEZWA NA LUCY WAKATI WA MAHAFALI YA KUPATA GAMBA


                                                                CATHY NA LUCY



                                             
                                                SIBONIKE, HANNAH NA CATHERINE
                                       HANNAH MAYIGE       NA CATHERINE NYONI
                                                            MR AND MRS MAYIGE

RAIS JAKAYA KIKWETE AMEWAAPISHA MAJAJI 14 IKULU LEO.





Rais JAKAYA KIKWETE amewaapisha MAJAJI 14 ambao wameteuliwa hivi karibuni katika hafla fupi iliyofanyika IKULU jijini DSM hafla amabyo imeudhuriwa na viongozi na wadau mbalimbali wa sekta ya mahakama.




Majaji KUMI na WATATU  walioapishwa wanatarajiwa kwenda kufanya kazi MAHAKAMA KUU na JAJI mmoja ni wa MAHAKAMA ya RUFANI.




MAJAJI wa Mahakama kuu walioapishwa ni PAUL KASTUS , LAMECK MLACHA ,SALIMA CHIKOYO, ISAYA KWEKA  ADAM MAMBI,ISSA MAIGE, REHEMA KEREFU , JULIUS MALABA na SILUS MATUPA.




Wengine ni LUCIA GAMUYA, BIN HAJI SHABAN, VICTORIA LYIMO MAKANI, na WIRFRED PETER ambapo jaji RICHARD MZIRAY ameapishwa kuwa jaji wa mahakama ya Rufani.

WATU 30 WAMEKUFA NCHINI INDIA



 Watu 30 wamekufa na wengine 25 kujeruhiwa katika jimbo la MADHYA PRADESH nchini INDIA, baada ya treni mbili za abiria kupinduka. Treni hizo zimepinduka, baada ya mataruma ya reli kusombwa na maji, kutokana na mafuriko makubwa yaliyoikumba nchi hiyo.



Mabehewa yaliyokuwa yakikokotwa na treni hizo mbili yalipinduka, na waokoaji wamekuwa wakiendelea na zoezi la kuwanasua watu walionasa katika mabehewa ya treni hizo, usiku kucha wa kuamkia leo.



Mvua za msimu zilizokuwa zikiendelea kunyesha mfululizo kwa wiki mbili nchini INDIA, zimesababisha maeneo mengi kuwa chepechepe, na hivyo hata mataruma ya reli kushindwa kuhimili uzito wa treni. Shirika la reli la INDIA limesema kuwa, limekuwa likifanya ukaguzi wa mara kwa mara wa reli zake.



Hata hivyo kuna habari kuwa, kingo za bwawa moja kubwa lililoko karibu na njia za reli zilipasuka na kufanya maji yake kusambaa, hivyo na hivyo kutatiza njia za reli. Wakati huohuo




Umoja wa Mataifa umesema, raia wapatao elfu TANO wameuawa nchini AFGHANISTAN katika kipindi cha miezi sita iliyopita. Taarifa iliyotolewa na umoja huo inasema watu waliokufa zaidi nchini humo ni wanawake na watoto.




Mapigano yanayoendelea nchini AFGHANISTAN ni moja kati ya sababu za vifo nchini humo, huku kundi la wapiganaji wa TALEBAN, likishutumiwa. Mtu mmoja aliyehojiwa anasema, mapigano hayo yamesababisha raia kushindwa kupata huduma muhimu za kibinadamu.




Thursday, 5 February 2015

KIKAO CHA KWANZA CHA BODI YA MRADI WA KILIMO CHA UMWAGILIAJI GEREZA KIGONGONI – BAGAMOYO KATI YA SHIRIKA LA MAGEREZA NA KAMPUNI YA TARBIM CHAFANYIKA LEO MJINI BAGAMOYO

unnamedX1 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tarbim, Bw. Baddal Calikusu akitoa maelezo mafupi kabla ya Ufunguzi wa Kikao cha kwanza cha Bodi ya Mradi wa Ubia wa Kilimo cha Umwagiliaji unaotarajiwa kuanza rasmi kutekelezwa katika eneo la Magereza, Gereza Kigongoni Bagamoyo(kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Magereza, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, John Masunga. Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Green Park iliyoko Bagamoyo. unnamedX3Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tarbim, Bw. Baddal Calikusu (aliyesimama) akitoa utambulisho kwa wajumbe wapya wa Bodi kabla ya Ufunguzi wa Kikao cha kwanza cha Bodi ya Mradi wa Ubia wa Kilimo cha Umwagiliaji unaotarajiwa kuanza rasmi kutekelezwa katika eneo la Magereza, Gereza Kigongoni Bagamoyo . unnamedX4Mpimaji Ardhi Mwandamizi wa Jeshi la Magereza,Mrakibu Msaidizi wa Magereza Habibu Yusuph akiwaonesha wajumbe wa Bodi mchoro wa Ramani katika mradi wa ubia wa Kilimo cha Umwagiliaji cha Gereza Kigongoni kati ya Kampuni ya Tarbim na shirika la Magereza.MAGEKamishina Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Gideon Nkana akiwa na Wajumbe wengine wa Bodi ya mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji Gereza Kigongoni wakikagua eneo la Mradi utakapotekelezwa unnamedX5 Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tarbim, Bw. Baddal Calikusu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya mradi wa Kilimo cha Umwagiliaji Gereza Kigongoni mara baada ya Kikao cha kwanza kilichofanyika katika Hoteli ya Green Park iliyopo Mjini Bagamoyo (wa kwanza kulia) ni Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Magereza Gideon Nkana(wa tatu kulia) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Magereza,Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Magereza John Masunga(

SERIKALI KUDHIBITI UJANGILI WA BIASHARA HARAMU MAZAO YA MALIASILI

mgi
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mahmoud Mgimwa akijibu swali bungeni.
……………………………………………………………………………………
Na Lorietha Laurence-Maelezo,Dodoma SERIKALI imejidhatiti katika kudhibiti ujangili na biashara haramu ya mazao ya maliasili kwa kuridhia na kutekeleza mikataba minne ya kudhibiti ujangali wa tembo na unaovuka mipaka na kulinda mapori ya akiba.

Kuingia kwa sekta ya afya katika BRN kunaleta matumaini mapya

Mtendaji Mkuu wa PDB Bw. Omari Issa akielezeaumuhimu wa sekta ya Afya kuingia BRN kuungana na sekta nyingine zilizotangulia zinazoendelea kuzaa matunda

TUPE MAONI YAKO