Sunday, 24 March 2013

MWENDESHA PIKIPIKI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI......WANANCHI WAPANDWA NA HASIRA NA KUMUUA ASKARI HUYO

 Wananchi wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamemwua askari mmoja na kumjeruhi mwingine kwa kutumia mawe, baada ya askari hao waliokuwa doria, kumwua kwa kumpiga risasi mwendesha pikipiki (bodaboda).

Askari Polisi, PC Yohana namba 7771 alipoteza uhai katika eneo la Ngwinde kutokana na waendesha pikipiki hao kushikwa na hasira za kuuawa kwa mwenzao aliyetambulika kwa jina la Makisio Ngonyani (27), mkazi wa kijiji hicho, na hivyo kuamua kupiza kisasi.

Akizungumza na kipindi cha Radio One Stereo Nipashe, Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, Deusdedith Nsimeki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo jana majira ya saa 8 mchana na kusema kuwa askari polisi wakiwa katika sare zao, walikuwa wamemfuatilia mwendesha pikipiki aliyekuwa amevunja sheria kwa kubeba abiria wawili na aliposimamishwa alikaidi.
 Baada ya kumkamata ndipo iliyopotokea purukushani ambapo risasi iliyofyatuliwa na askari ilimjeruhi mtu mmoja kidoleni kabla ya kumpata marehemu kwenye paji la uso, na kusababisha kifo chake papo.

Kamanda Nsimeki amesema, baada ya kuona hivyo, wananchi walichukua miti mikavu na mawe na kuanza kumshambulia PC Yohana na kusababisha kifo chake.

Askari aliyejeruhiwa, Konstebo Venance Kamugisha yupo katika hospitali ya Songea Mjini, kwa matibabu ya majeraha aliyoyapata kichwani na kusababisha kupoteza damu (bleeding excessively).

Kamanda Nsimeki amesema jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi ili kupata ripoti kamili.

Rais wa Jamuhuri ya watu wa China Xi Jinping kuanza ziara ya kihistoria nchini leo.

Na Eeuteri Mangi na Hussein Makame – Maelezo.
Rais wa Jamuhuri ya watu wa China Xi Jinping (pichani) anataraija kuanza ziara ya kihistoria nchini tangu kuapishwa  kwake kuitumikia  nchi hiyo ambapo katika ziara hiyo atasaini mikataba 17 ya ushirikiano wa  kiuchumi kati ya Serikali za Tanzania na nchi hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe alisema kuwa  ziara hiyo ni ya kwanza barani Afrika  kwa Rais huyo mpya wa China baada ya kuchaguliwa kuliongoza taifa hilo Machi 14 mwaka huu.
Lengo la ziara hiyo ambayo itaanza tarehe 24 hadi 25 Machi mwaka huu ni kukuza uwekezaji  na biashara baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Baadhi ya Mikataba hiyo itahusiana na uboreshaji wa sekta ya viwanda, kilimo hasa cha tumbaku ikiwemo kuwatafutia soko wakulima kutoka mikoa ya Tabora na Ruvuma ili waweze kuuza zao hilo katika soko la China.
Waziri Membe alisema kuwa; “Mikataba mingine ni ya kulipatia Shirika la Utangazaji Tanzania zana za kufanyia kazi na kuandaa mazingira ya ujenzi wa bandari ya Bagamoyo itakayounganishwa na reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), reli ya kati na barabara”.  
Rais Xi Jinping pia atazindua na kukabidhi rasmi kituo cha Mikutano cha  Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere  chenye ghorofa tatu na kumbi nne za mikutano  zenye uwezo  kupokea washiriki zaidi ya 1800 kilichogharimu dola za kimarekani milioni 29.7 zilizotolewa na Serikali ya China kwa lengo la kumuenzi Mwalimu Nyerere.
Waziri huyo alisema kuwa baada ya kufika nchini Rais Xi Jinping atazungumza na mwenyeji wake Rais Dk. Jakaya Kikwete pamoja na Viongozi Waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye atahudhuria dhifa ya kitaifa Ikulu Jijini Dar es salaam.
Siku ya pili ya ziara yake Rais Jinping  atazungumza rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein pamoja na ujumbe wa viongozi waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri Membe aliongeza kuwa Rais Jinping atatoa hotuba maalumu kwa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla na  kuzungumzia sera ya Serikali mpya ya China kwa bara la Afrika ambayo itahudhuriwa na watu kutoka kada mbalimbali ikiwemo Viongozi na Maafisa Waandamizi wa Serikali, Wahadhiri wa Vyuo Vikuu,Wabunge, Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia na Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.
“Hotuba hiyo ya Rais wa China ataitoa kwa lugha ya Kichina na kutafsiriwa  kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili ili iweze kuifika dunia nzima, hivyo tunaviomba vyombo vya habari nchini vichukue fursa hiyo kuwa vya kwanza kuutangazia Ulimwengu” alisema Waziri Membe.
Ziara hiyo ya Rais wa Jamhuri ya Watu wa China  ni muendelezo wa uhusiano mzuri kati ya nchi hiyo na Tanzania ulioasisiwa na viongozi  wa mataifa hayo mawili, yaani Mao Zedong wa China na  Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania.
Rais Jinping ataondoka nchini Machi 25 saa 10:40 jioni kuelekea nchini Afrika Kusini kuhudhuria mkutano wa tano wa Wakuu wa Nchi zinazokuwa kwa kasi kiuchumi ambazo ni Brazil, Urusi, India, China na Afrika ya Kusini (BRICS).

TAIFA STARS YAWAZABA LIONS OF THE ATLAS

Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wamewainua watanzania kwa kumzaba Morocco mabao 3-1 katika mechi ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia.

Mabao ya Taifa Stars yametupiwa na Thomas Ulimwengu katika dakika ya 46 na Mbwana Samatta alizifumania nyavu katika dakika za 67 na 80.

Bao pekee la Lions of The Atlas limefungwa katika dakika ya 90 ya mchezo huo ambao umechezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Pia katika mechi hiyo mchezaji wa Morocco Abderrahim Chakir alionyeshwa kadi nyekundu kufuatia kucheza vibaya.

Kwa matokeo hayo Stars inaendelea kushika nafasi ya pili ikiwa na alama 6 kutokana na Ivory Coast jana kumnyuka Gambia mabao 3-0 na kuwa na pointi 7 ikipisha alama moja tu na tembo hao wa Afrika.

Thursday, 21 March 2013

ZIARA YA RAIS DK. SHEIN MKOANI PEMBA


DSC_0015
Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akipokea Taarifa ya ujenzi wa kituo cha Afya
Tasini  Kiwani kutoka kwa Mwalimu Abdalla Juma Mustafa, baada ya
kukagua maendeleo ya Ujenzi wa kituo hicho,akiwa katika ziara ya
Wilaya ya Mkoani Pemba jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
DSC_0011Wananchi wa Tasini  Kiwani wakimsikiliza Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipofika
kuwasalimia baada ya  kukagua maendeleo ya Ujenzi wa barabara ya
vijiji hivyo  akiwa katika ziara ya Wilaya ya Mkoani Pemba jana.[Picha
DSC_0028 Baadhi ya wanafunzi na Wazee wa wakimsikiliza Rais wa wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein,alipokuwa akizungumza nao alipokagua ujenzi wa kituocha Afya na
barabara ya Tasini Kiwani ,akiwa katika ziara ya Wilaya ya Mkoani
Pemba jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] DSC_0030Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto) na Viongozi wengine wakiitikia
dua baada ya kukamilika kwa harambeee aliyoiitisha kuchangia ujenzi wa
Kituocha Afya Tasini Kiwani Wilaya ya Mkoani Pemba,akiwa katika ziara
ya kikazi ndani ya Mkoa huo. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
DSC_0039Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) alipofika kukagua wagonjwa
akianza na Mzee Hassan Kombo,aliyepata ajali ya vespa akiwa katika
Hospitali ya Mkoani Pemba,katika ziara ya   kikazi ndani ya Mkoa huo.
[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
DSC_0043Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alipofika kukagua wagonjwa
katika Hospitali ya Abdalla Mzee,Mkoani Pemba,pichani Dk.
Shein,akimuangalia Mtoto Husna Mohamed Kombo,(kichanga) akiwa na Mama
yake  Riziki Haji,mtoto huyo anasumbuliwa na kitovu,Rais akiwa
kisiwani Pemba kwa Ziara ya kikazi ndani ya Mkoa wa Kusini . [Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]

DSC_0095 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto) akipatra maelezo
Kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Salum Maulid, (Kibanzi) alipotembelea matengenezo
makubwa ya Ikulu Ndogo ya Mkoani Pemba,alipokuwa katika ziara ya Mkoa
wa Kusini Pemba jana. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Thursday, 14 March 2013

TUJIJENGEE MAZINGIRA YA KUPIMA AFYA ZETU


Siku ya mmiliki wa blog ya demashonews alipochukua jukumu la kupima afya yake kwa hilayali katika kituo cha afya kilichopo Madaba songea vijijini Mkoani Ruvuma.
Ni uso wenye furaha tele baada ya kupewa majibu yake " wito wangu kwa watanzania wenzangu kuwa na  tabia ya kupima afya zetu mara kwa mara tusingojee pale unapokuwa na tatizo ndipo ukapime afya yako" hayo ndio maneno aliyoyasema mmiliki wa blog ya demashonews baada ya kupima afya .

CHINA YAITABIRIA TANZANIA KUPIGA HATUA



1. KINANA NA UJUMBE WAKE KWENYE MNARA WA PILI DUNIANI KWA UREFUaMtumishi katika mnara wa Canton, mrefu kuliko yote nchini China na watatu duniani kwa urefu, Sarah Xie, akimuonyesha mandhari ya jiji la Guangzhou, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, wakati Kinana na ujumbe wake walipopanda hadi mwisho mnara huo wenye urefu wa zaidi ya futi 100, Machi 13, 2013. Wengine Kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine shigella. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo). 3. KINANA NA UJUMBE WAKE NDANI YA MNARAaKatibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakitazama maumbo ya mandhari ya mji wa Guanzhou, China, yaliyopo ndani ya mnara wa Cnton wenye urefu wa zaidi ya mita 100, walipotembelea mnara huo, Machi 13, 2013.  Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo).
10. DK. MIGIRO NA MAOFISA WA IDARA YA MAMBO YA NJE WA DONGGUANSABINA LIU (L) NA SARAH XIEaKatibu wa NEC, Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa mjini Magharibi, Yussuf Mohamed Yusuf wakitaza bidhaa zinazouzwa kwenye kilele Mnara wa Canton ambao ni mrefu kuliko yote nchini China ukiwa na urefu wa zaidi ya mita 100, mjini Guangzhou, China. Dk. Asha-Rose Migiro na Yusuf ni miongoni mwa viongozi walioambatana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana katika ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo).
13. KINANA NA MIGIRO WAKIWA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WA-TZ WAISHIO CHINA. (L) DAVID CHAMALA (KTB), JOHN LUHEMBA (MKT)-L, ABRAHAM MERISHANI MAKAMU MKT NA ABUBAKAR MWINYI KATB MSAIDIZIaKatibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wanachama wa Jumuia ya watanzania waishio nchini China

NA BASHIR NKOROMO, DONGGUAN,CHINA

CHAMA Cha Kikomunisti cha China (CPC) kimeeleza matumaini yake kwamba upo uwezekano wa Tanzania kupiga hatua kubwa kichumi kama inajikita kwa dhati katika kuzitumia rasilimali ilizonazo ikiwemo ardhi.
Hayo yalisemwa Machi 13, 2013 na Kamishna wa Maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), jimbo la Donguan, China,  Cuo Jian, wakati akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake, katika hoteli ya Exhibition Internation mjini hapa.
Jian ambaye pia ni Meya wa jiji la Donguan, alisema, Tanzania kama zilivyo nchi kadhaa za Afrika, inaweza kupiga hatua kiuchumi ikiwekeza juhudi zake katika kuzitumia rasilimali ilizonazo kwa kuwa rasilimali ndiyo msingi wa kwanza katika kuinua uchumi wa nchi yoyote.
Alisema, anatambuwa kwamba Tanzania ni moja ya nchi za Afrika zenye ardhi kubwa, hivyo haina budi juhudi zake za kuinua uchumi kuzielekeza katika rasilimali hiyo ikiitumia kwa kilimo cha kisasa, kujenga viwanda na vitegauchumi mbalimbali ambavyo vitachochea kukua haraka kwa uchumi.
“Hata hivyo nawapongeza Tanzania, kwa hatua mliyofikia sasa katika kukuza uchumi, asilimia sita ya GDP, inaridhisha, la msingi serikali  kuongeza juhudi na kuwahamasisha wananchi kushiriki katika juhudi hizo”, alisema, Jian.
Akijibu swali na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu, ambaye yupo kwenye msafara wa Kinana katika ziara hiyo, Titus Kamani aliyetaka kujua ni nini hasa China ilifanya hadi kuufanya uchumi wake ukue haraka na kuwa nchi ya pili dunia kwa maendeleo, Jian alisema, China imefikia mafanikio hayo kutokana na kuamua kuwekeza kwa nguvu zake zote kwenye rasilimali ya ardhi.
“Zipo njia nyingi za kuweza kuinua uchumi wa  nchi yoyote, juhudi hizo baadhi zinafanana na nyingine ni tofauti kutokana na nchi na nchi, lakini sisi (Wachina) tulifahamu kwamba tuna ardhi kubwa sana, hivyo tukaamua kuimua rasilimali hii kwa kila namna iliyo bora. Licha ya eneo kuwa kubwa lakini tumehakikisha hakuna eneo linaloachwa bila faida”, alisema.
Kwa upande wake Kinana aliupongeza uongozi wa China chini ya chama cha CPC na wananchi wa nchi hiyo kwa kuweza kufanikisha kuinua uchumi wa nchi hiyo kwa kiwango kibwa cha sasa.
“Bila shaka ni uchapakazi usio na kikomo na wakujituma sana kwa pamoja kati ya serikali na wananchi ndiyo maana mmefanikiwa hivi, napenda kuchua fursa hii niwapongeze kwa dhati kwa mafanikio haya, nasi kama nchi rafiki tunapata kiu kubwa kuhakikisha tunafika mlipo au angalau kuwakaribia”, alisema Kinana.
Kinana yupo nchini China akiambatana na ujumbe wa viongozi na maofisa wa Chama kwa ajili ya ziara ya mafunzo, katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kisiasa, na pia kudumisha urafiki wa kindugu wa siku nyingi kati ya Chama Cha Mapinduzi na Chama Cha Kikomunisti cha nchi hiyo.
Katika ziara hiyo Kinana amefuatana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar), Vuai Ali Vuai, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Khadija Aboud, Katibu wa NEC, Siasa na Uhuaisno wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martine Shigela, Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi, Khamis Suleiman Dadi na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi Mohammed Yusuf Mohamed.
Wengine ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa,  Jesca Msambatavangu, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu Titus Kamani, Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na maofisa wa Chama. ziara hiyo
Kinana anafanya ziara  hiyo kutokana na mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China, na anafanya ziara hiyo ikiwa ni ya kwanza kuifanya nje ya nchi, tangu alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Oktoba mwaka jana mjini Dodoma
Chanzo cha habari http://www.fullshangweblog.com

Monday, 11 March 2013

MSAADA WAKO UNAHITAJIKA ILIKUWEZA KUOKOA UHAI WA MTOTO SIMON MLOPE



Hivi ndivyo hali ya mtoto Simon Mlope ilivo kwa sasa
 Mtoto Simon Mlope akiwa na mama yake ambaye anaitwa Amina Ally
Angalia Video ya  mtoto Simoni Mlope akiwa na Mama yake. 
 

Mtoto simon Mlope mwenye umri wa miaka 11 mkazi wa eneo la mahenge katika manispaa ya songea mkoani Ruvuma amelazimika kukatisha masomo yake ya shule ya msingi akiwa darasa kwanza  kutokana na mototo huyo kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo .
Awali tulitoa habari za mtoto huyu akiomba msaada lakini hadi sasa bado hajapata msaada wowote ule wa kuweza kuokoa maisha yake. Nahivi sasa hali ya mtoto huyu inazidi kuwa mbaya kiafya .

 Mtoto simon Mlope alikubwa na ugonjwa  moyo  tangu mwaka 2001 mara baada ya kuzaliwa na kugundulika kuwa  moyo wake una tundu hali ambayo inasababisha  kuvuta pumzi kwa shida.
Mama wa mototo  simon mlope anayeitwa AMINA ALLY  anawaomba watanzania kumsaidia mtoto  wake fedha za matibabu Baada ya kuambiwa na madaktari kuwa simon anatakiwa kwenda nchini  india kutibiwa,baada ya kupata rufaa kutoka muhimbili mwaka 2006  huku familia yake ikiwa haina uwezo kabisa.

Majirani wa familia ya simon nao wanasema kuwa mototo simon anahitaji msaada wa haraka kwa kuwa hali yake sio nzuri na kuwaomba watanzania wamsaidie.
Kinachosikitisha zaidi baba wa mtoto huyo  anayejulikana kwa jina la SIMON MLOPE  ameondoka nyumbani hapo tangu mwaka 2011 na hajulikani aliko kwa sasa, ingawa mwanzoni alisema yuko nchini Msumbiji.
Kwa anayeguswa na tatizo hili na anataka kumsaidia  SIMONI MLOPE  atumie simu namba  0752732290
Picha na habari kwa hisani ya http://demashonews.blogspot.com

TUPE MAONI YAKO