Saturday 30 August 2014

WAFANYAKAZI 45 WA HALMASHAURI YA WILAYA YA TUNDURU WANUSURIKA KUFA BAADA YA BASI WALILOKUWA WAKISAFIRIA KUPINDUKA.


ZAIDI ya Wafanyakazi 45 wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru Mkoni Ruvuma wamenusulika kufa baada ya Basi lenye namba za usajiri T 966 AXQ mali ya  kampuni ta Ng’itu Expres walilokuwa wakisafiria kupinduka.

Sambamba na tukio la ajali hiyo taarifa zinaeleza kuwa watu wane (4) wamejeruhiwa kutokana na kuumia sehemu mbalimbali za miili yao  kukimbizwa katika Hospitali ya serikali ya Wilaya ya Tunduru.

Wakiongea kwa njia ya simu baadhi ya manusula hao walisema kuwa ajali hiyo ilitokea katika eneo la Lumesule mpakani mwa Wilaya zaTunduru Mkoni Ruvuma na Mangaka Mkoani Mtwara.

Kwamujibu wa taariha hizo watumishi hao ambao walifuatana na wakuu wao wa idara walikuwa wana kwenda Wilayani Masasi Mkoani Mtwara kwa ajili ya kushirki katika Mazishi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa hamalshauri yao Marehem Robert Nehatta.

Akifafanua taarifa za tukio hilo Dkt. Jacob Madondola ambaye ni kati ya manusula hao alieleza kuwa mbali na gari hilo kuwa katika mwendo kasi chanzo cha ajali hiyo kilisababishwa na kuchomoka kwa Stelingi na kumshinda dereva.

 Katika taarifa hiyo mashuhuda hao waliwataja watu waliojeruhiwa kaatika ajali hiyo kuwa ni Bw. John Kamwela (afisa Biashara wa Halmashauri hiyo), Bi. Malisela Mapunda(afisa manunuzi wa halamsahauri hiyo), Mwl. Joseph Makina ( msaidizi wa afisa elimu wa Shule za Sekondani Wilayani humo) pamoja na Bw.Joseph Mtauchila (Mkaguzi wa ndani).

Mganga mfawidhi katika Hospitali ya Wilaya Dkt. Joseph Ng’ombo amekiri kuwapokea majeruhi hao na kuwapatia matibabu na kwamba halizao zinaendelea vizuri. 

Akizungumzia tukio hilo kwa njia ya Simu, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Bw. Chande Nalicho  ametoa pole kwa wahanga hao alisema kuwa ajali hiyo imetokea katika mazingira ya uzembe wa wamiriki wa gari hilo kutolifanyia uchunguzi wa kina wa mara kwa mara.

Alisema Maremu Robert Nehatta alifariki Dinua usiku wa kuamkia Agost 26 mwaka huu akiwa katika Hospitali nchini India ambako alienda kwa ajili ya matibabu ya Figo yaliyokuwa yakimsumbua.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO