Monday 31 December 2012

2013 Inspiration!

                                                                       Gorgeous Haaa!


What a beautiful collection
                           Start planning for your fabulous look and Wedding Spot will be there to facilitate.

                                           Emerald Green at Wedding Spot

Thinking ahead for our brides is our duty. You can find Emerald green wedding gowns at Wedding Spot that can be worn by 2013 brides; depending on the wedding colour theme or can be worn in the Islamic weddings ( Aqdi) as two in one gown!

Have you ever thought that wedding dresses go along with fashion trends...? Can you look gorgeous in the Emerald Green? Pop up at Wedding Spot, we keep spotting the best for the best Brides...!!! If you can not make a surprise shout for the superb dresses and accessories, you will breath so deeply...!! Sample dresses to be posted shortly...........

MATUNDA YAHARIBIKA KWA KUKOSA VIWANDA VYA KUTENGENEZA JUISI MKONI RUVUMA

  Embe ambazo zimedondoka na  zimeachwa   zikiharibika kutokana na uwingi wa tunda hili la msimu .

RAIS KIKWETE AMJULIA HALI PADRI AMBROS MKENDA ALIYEPIGWA RISASI ZANZIBAR

  
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali Padri Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae mjini Zanzibar anayeuguza majeraha katika taasisi ya mifupa ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) jijijini Dar es salaam leo Jumamosi Dsemba 29, 2012 kufuatia kupigwa risasi sehemu za mdomoni na watu wasiojulikana mapema wiki hii wakati akisubiri kufunguliwa geti la nyumbani kwake maeneo Kitomondo Mjini Zanzibar akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha akiwa pekee yake. Rais Kikwete amempa Padri Mkenda pole nyingi na kumuombea apate nafuu haraka.
 
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimsikiliza Padri Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae mjini Zanzibar anayeuguza majeraha katika taasisi ya mifupa ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (Moi) jijijini Dar es salaam leo Jumamosi Dsemba 29, 2012 kukupigwa risasi sehemu za mdomoni na watu wasiojulikana mapema wiki hii wakati akisubiri kufunguliwa geti la nyumbani kwake maeneo Kitomondo Mjini Zanzibar akiwa ndani ya gari aliyokuwa akiendesha akiwa pekee yake. Rais Kikwete amempa Padri Mkenda pole nyingi na kumuombea apate nafuu haraka.
PICHA NA IKULU

YAKIWA YAMEBAKI MASAA MACHACHE KUZIMWA KWA MITAMBO YA ANALOJIA HIVI NDIVYO HALI ILIVYO MIDA HII KWENYE OFISI ZA STAR TIMES MWENGE

Baadhi ya wakazi wa jiji la Dar wakiwa wanasubiria Kuingia ndani ya ofisi ya Star Times Mwenge kutokana na wateja kujaa ndani ya ofisi hiyo kwaajili ya kununua ving'amuzi na kupelekea wateja hao kuingia kwa kusubiriana. Ikumbukwe kuwa  mnamo tarehe 23 februari 2012  Wizara ya Sayansi na Teknolojia kupitia Mamlaka ya Mawasiliano nchini TCRA ilitangaza kusitisha urushaji wa matangazo ya televisheni kwa kutumia teknolojia ya analojia kwenda katika mfumo mpya wa digitali kufikia tarehe 31 Disemba 2012 saa sita na dakika moja usiku
Baadhi ya Wakazi wa Jiji la Dar wakiwa wamekaa nje ya ofisi ya Star Time Mwenge wakisubiria wateja wengine waliopo ndani wapungue ili na wao waweze kuingia na kununua ving'amuzi vya kampuni hiyo.
 Kijana akitoka kununua king'amuzi cha Kampuni ya Star Times tayari kwa kupokea matangazo ya televisheni kwa njia ya digitali
Mkazi wa Jiji la Dar  akiwa tayari kashajinunulia king'amuzi cha Kampuni ya Star Time tayari kwa kupokea matangazo kwa njia ya digitali ambapo Tanzania inaingia kwenye mfumo mpya wa urushaji wa matangazo ya televisheni kupitia mfumo wa digitali. Kufikia saa sita na dakika moja usiku wa leo Serikali imeagiza wamiliki wote wa vituo vya televisheni kuzima mitambo yao inayotumia teknolojia ya analojia na kuwasha mitambo mipya inayotumia teknolojia ya Digitali.

MAGHALA YA KUHIFADHIA BIDHAA ZA WAFANYA BIASHARA WA MWANJELWA YATEKETEA KWA MOTO

Maghala ya kuhifadhia bidhaa mbali mbali za wafanya biashara wa mwanjelwa Mbeya yameteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo maghala hayo yapo maeneo ya uwanja wa ndege wa mwanjelwa
Wanausalama wakiwa makini na vibaka ambao walitaka kuvamia eneo hilo la moto kutaka kupora mali kujifanya wanaokoa mali hizo
Hakika kikosi cha zimamoto cha jiji la mbeya wakishirikiana na kikosi cha zimamoto uwanja wa ndege wa songwe walijitahidi kuuzima moto huo ingawa mara kwa mara waliishiwa maji kutokana na uwezo mdogo wa magari hayo kubeba maji ya kuzimia moto
Moja ya gari ya kampuni ya jambo ikiungua moto katika maghala hayo
Moja ya wafanyabiashara hao ambaye anamizigo yake katika maghala hayo akikatazwa na mwanausalama kwamba asiende kmuokoa mali zake kwani moto ni mkubwa awaachie kikosi cha zimamoto kifanye kazi yake
Mfayabiashara huyo haamini mcho yake huku akilia akiona bidhaa zake zikiteketea kwamoto
Kama kawaida kmufa kmufaana hapa vibaka wakigombea sahani na masufuria kwenye box
Hakika jeshi la polisi linastahili pongezi kwa kazi kubwa ya kuokoa mali za wafanyabiashara ambao bidhaa zao zilikuwa katika maghala hayo hapa polisi wakiwa wamemshika kibaka aliyetaka kuiba mafuta ya kupikia
Kwakweli ilikuwa hatari kwani vibaka walikuwa wanarusha mawe kwa polisi na kwa baadhi ya magari hapa hili gari ikitoka katika ghala hilo likiwa limevunjwa kioo cha mbele
Baadhi ya wananchi wengi wakiwa katika tukio hilo
Haya si maji bali ni mafuta ya kula ambayo yamemwagika baada ya blastiki kuyeyuka kwa moto
Asubuhi hii moto ndiyo unaishia
Hali halisi baada ya kuungua kwa maghala hayo hili si tope mali ni mafuta ya kula yaani mafuta ya kupikia
Baadhi ya wafanyabiashara wakijaribu kuokota baadhi ya mabaki ya bidhaa zao zilizopona katika moto huo
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Athuman Diwani akiongea na waandishi wa habari leo amesema anawapongeza sana wakazi wa Mbeya hasa wale wa maendeo yanayozunguka maghala yalioteketea kwa mtoto kwa ushirikiano wao kuwezesha kuokoa baadhi ya bidha za wafayabiashara licha ya vijana wachache kutaka kuiba na kutupa mawe askari wake ili wafanye uhalifu wa kupora bidhaa zilizokuwa zinaokolewa hapo mpaka sasa vijana wawili wamekamatwa kwa kutupiaaskari mawe na kuiba bidhaa zilizokuwa zinaokolewa
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza kamanda diwani

Saturday 29 December 2012

Changamoto Ya Usafiri Sumbawanga

 Sehemu ya barabara ikiwa imeharibika baada ya mvua kunyesha katika kijiji cha kianda,Sumbawanga
Basi likiwa limekwama,jana asubuhi kijiji cha Kianda Sumbawanga
 'Greda' likisaidia kuvuta basi baada ya kukwama kwenye tope.Jana mchana,Kianda-Sumbawanga

MKUTANO WA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO TASWA WAFANYIKA BAGAMOYO LEO

Mwenyekiti wa kamati ya Kusaidia timu ya Taifa ya Vijana Serengeti Boys Bw. Ridhiwan Kikwete  akifungua mkutano mkuu wa chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA unaofanyika kwenye Hoteli ya Kiromo View Bagamoyo mkoani Pwani ambao unajadili mambo mbalimbali ya Maendeleo na changamoto zinazokabili chama hicho.
Waanishi wa habari za michezo ambao ni wanachama kutoka vyombo mbalimbali nchini wanahudhuria mkutano huo ambao ni wa siku moja.
Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA Bw. Juma Pinto akimkaribisha mgeni rasmi ili kufungua mkutano huo leo asubuhi unaofanyika kwenye  hoteli ya Kiromo View Bagamoyo.
 
Katibu wa Chama cha Waandishi wa habari za michezo TASWA Bw. Amir Mhando akizungumza katika mkutano huo, kutoka kulia ni Makamu Mwenyekiti wa TASWA Maulid Kitenge, Mwenyekiti Juma Pinto, Mgeni rasmi Ridhiwan Kikwete na kushoto ni George John Katibu Msaidizi.
 
Mtaalam wa SACCOS kutoka Manispaa ya Ilala Bw. Luambano akitoa mada kuweka na kukopa kwa waandishi wa habari wanachama wa TASWA waliohudhuria katika  mkutano huo
 
Kutoka kulia ni waandishi wakongwe Mwina Kaduguda, Mzee Wlly Chiwango na Mzee Salim Said Salim kutoka Zanzibar wakiwa katika mkutano huo.
 
Kutoka kulia ni Shafii Dauda, Erasto na Ibrahim Masoud wakiwa katika mkutano huo.
 
Kutoka kulia ni Elizaberth Mayemba , Timzo Kalugira na Crala Alphonce wakifuatilia mada katika mkutano huo.
 
Kutoka kushoto ni Elius Kambili, Alfred Lucas na Salum Jaba wajumbe wa kamati ya utendaji ya TASWA wakiwa katika mkutano huo.
 
Kutoka kulia ni Mgaya Kingoba, Salum Jaba, Richard Mwaikenda na Tulo Chambo wakifuatilia mada katika mkutano huo.
 
Wajumbe mbalimbali wakihudhuria mkutano wa Chama cha Waandishi wa habari za michezo TASWA kwenye hoteli ya Kiromo View mjini nje kidogo ya mji wa Bagamoyo mkoani Pwani .

TUPE MAONI YAKO