Thursday 30 October 2014

MAMA TUNU PINDA ALIPOTEMBELEA RUVUMA KUZUNGUMZA NA WANAVIKOBA NA HAPO NI KATIKA VIWANJA VYA MAJIMAJI AKIPOKEA MAANDAMANO









UPEPO MWINGINE BWANA NOUMA

UPEPO mkali uliozuka katika Kijiji cha Molandi kilichpo katika Kata ya marimba Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma Umeezua Nyumba 10 na kuziacha familia hizo zikiwa hazina makazi.

Aidha taarifa za awali zinaeleza kuwa katika tukio hilo upepo huo umeezua nyuma 7 za bati na nyumba 3 zilizotuku zimeezekwa kwa nyasi na umesababisha hasara ya kumla ya Shiringi Milioni 11.925,000.
Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa zuruba hilo liliwakumba wakazi wa Kijiji hicho Oktoba 12 mwaka huu majira ya saa 7 mchana na kuzusha taharuki kubwa kwa wakazi wa kijiji hicho.

 Taarifa hiyo inafafanua kuwa Sambamba na tukio hilo pia upepo huo ilisomba moto ambao ulisababisha ungua kwa nyasi zilizotuka kuezekea baadhi ya nyumba pamoja na kuunguza uwanja wa timu ya Kijiji hicho ya Nyuki Fc.
Akiongea kwa njia ya simu Diwanai wa wa kata hiyo Bw. Msenga Saidi alidhibitisha kutokewa kwa tukio hilo na kuongeza kuwa kufutia tukio hilo wahanga kutoka katika kaya hizo hivi sasa wanahidhiwa katika nyumba za majirani ambao nyumba zao zilinusulika.

Bw. Msenga aliwataja wahanga wa tukio hilo kuwa ni Bw. Omary Jafari Mchali, Abdalah Said Manjolo, Abdalah Halifa Limbanga na Mohammed Omary Mangwila.

 Kwamujibu wa diwani huyo wahanga wengine ni Said Omari Yazidu, Ommari kazembe Nangwale,Mohammed Kazembe Nangwale, Mohammed Makunganya Mohhammed Juma wandale 

 Nae mwenyekiti wa kamati ya maafa,ulinzi na usalama Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Chande Nalicho pamoja na mambo mengine alisema kuwa baad ay atukio hilo kamati yake iliwatembelea wahanga hao na kuwapa pole.
Alisema wakiwa katika eneo hilo pia walizungumza na wahanga hao pamoja na kuwapatia ushauri wa kufuata hatua za ujenzi imara wa nyumba zao pamoja kupanda miti ya kujikinga ma majanga ya aina hiyo.
Mwisho

SAKAMIMBA TUNDURU MARUFUKU

SERIKALI Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma imepiga marufuku ngoma za Usiku ambazo zimekuwa zikichezwa na watoto wa Kike maarufu kwa jina la SAKAMIMBA.

Sambamba na marufuku ya ngoma hizo pia jamii imeaswa kuachana na utaratibu wa mila potofu za kuwacheza jando na unyago watoto wenye umri mdogo ili kuendelea kulinda maadili ya destuli za mwafrika. 
Aidha taarfa hiyo pia imewataka watendaji wa vijiji,kata na maafisa tarafa kuratibu, kusimamia na kuzuwia shughuli za Sherehe ambazo zitakuwa hazizingatii maadali katika maeneo yao.

Hayao yalisemwa na Mkuu wa Wilayab ya Tunduru Bw. Chande Nalicho wakati akiongea na wananchi wa Kijiji cha songambele kilichopo katika tarafa ya Nakapanya wilayani himo na akawataka wananchi kuhakikisha kuwa shughuli hizo zinaratibiwa na kutekelezwa kwa Watoto wenye umri mkubwa ikiwa ni tofauti na sasa ambapo wazazi na walezi hao wamekuwa wakiwacheza wakiwa na umri mdogo.

Akifafanua taarifa hiyo dc, Nalicho alisema kuwa mtindo wa wanafamilia hao kuwapeleka na kuwacheza unyago kwa watoto wa kike na jando kwa watoto wa kiume wakiwa na umri mdogo umekuwa ukidhalilisha utamaduni wetu.
Alisema kwani baada ya watoto hao wenye umri mdogo baada ya kumaliza mafunzo hayo huenda kutoa siri za mafunzo hayo kwa wenzao na kufanya majaribio kwa vitendo mambo yote waliyojifunza.

“mafunzo hayo ni hatari na nijanga kubwa hasa kwa watoto wa kike ambao baada ya kumaliza mafunzo hayo huenda kufanya majaribio kwa vitendo mambo yote waliyojifunza” alisema Dc, Nalicho.
Alisema kufuati jamii kuendelea kupuuza taratibu za kutekeleza wajibu wao katika malezi ya Watoto wao hasa wakike vitendo hivyo ndivyo ambavyo vimekuwa vikipelekea watoto wa kike kupata mimba wakiwa katika umri mdogo.
Mwisho
Wanafunzi  130 wa shule ya sekondari MBUNGA iliyopo katika kijiji cha NAIKESI kata ya KITANDA katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma Wameshindwa kumaliza kidato cha nne kwa kukatisha masomo yao kutokana na kupata mimba na utoro na kifo na kukariri darasa.

WATEJA WA NMB TAWI LA SONGEA WALIOJISHIDIA BAISKELI KATIKA SHINDANO LA WEKA NA USHINDE








TUPE MAONI YAKO