Sunday 31 March 2013

TANZANIA HAINA HISTORIA YA UMWAGAJI WA DAMU KWA RAIA WAKE HATA WAKATI WA KUDAI UHURU WAKE , ILA SASA TUNAONA DALILI ZA UMWAGAJI WA DAMU KWA BAADHI YA RAIA WAKE.

 Askofu Mkuu Dkt Norbert Mtega akibariki waumini baada ya Ibada ya PASAKA Kanisa kuu la Songea leo.
Waumini wakiwa katika Ibada ya PASAKA
 Waumini
 Kwaya ya DONBOSCO ambayo imekoleza ibada hiyo leo siku ya PASAKA
 Zifuatazo ni picha za umoja wa Wanamama Katoliki ( WAWATA) ,Wa Jimbo la Songea
 Kutoa vipaji akina mama ( WAWATA)

 Vipaji akina mama ( WAWATA )
Katika masomo ya Ibada ya PASAKA akina mama wa WAWATA wakipeleka Biblia ili kwenda kusoma na baadaye Injili.Aliyeshika Biblia menye gauni la kijani ni Bi. Cosensa Mbena na wa pili ni Bi Geni.
KATIKA Ibada ya PASAKA kwenye kanisa kuu la  Katholiki la Jimbo kuu la Songea la Mt.Mathias Mulumba Kalemba mjini Songea,ambao waumini wa kanisa hilo waliungana na wenzao Duniani kote kwa sherehe za PASAKA,
Hata hivyo alisema kuwa nchi ya Tanzania haikuwa na Historia ya umwagaji wa damu hata wakati wa kudai Uhuru wake,lakini kuna baadhi ya raia wamemwaga damu kutoka kwa watu wasio eleweka.
 
Hayo yametolewa katika mahubiri ya Askofu Mkuu wa Jimbo hilo,Dkt.Norbert Mtega katika Ibada ya sherehe za PASAKA leo,na kwamba ukombozi wa Yesu Kristu kwa kufa na kufufuka kwake uwe kwa watu wote wanao mwamini Mungu hata kama hawajabatizwa.
Aliwashukuru sana waandishi wa habari katika mchango wao wa kuandika na kuripoti uharibifu na vifo kadhaa vilivyo jitokeza katika nchi yetu na wengine  kupata vilema vya kudumu kama vile kutolewa macho.
 
Alisema kuwa waumini waende kumtangaza ufufuko wake wa  amani,upendo na mshikamano,bila ya kujali tofauti za Imani miongoni mwao,kwani wote ni wana wa Mungu.
Aidha alisema kuwa waumini wanatakiwa kuwa na Biblia mikononi mwao,nyumbani kwao na msalaba ambao ni ukombozi wao,kwani Biblia ni neon la Mungu la uzima ,nasio kama vitabu vingine.na kwamba wanawake wameonekana kuwa na mwamko wa kuwa na Biblia na kushiriki katika Jumuia ndogondogo.

Amewataka wanaume nao kushiriki katika uinjilishaji kwa kwenda kwenye Jumuiya ndogondogo ,pamoja na Biblia kama wanavyo fanya wanawake,ambapo Umoja wa Wanawake katoliki ( WAWATA ) Jimbo la Songea walitoa vipaji katiba Ibada ya PASAKA.
 
Chanzo http://ruralpresssongea.blogspot.com

Friday 29 March 2013

RAIS KIKWETE AFIKA ENEO LA TUKIO NA KUSHUHUDIA HALI HALISI YA KUANGUKA KWA JENGO LA GHOROFA 16 JIJINI DAR,HALI YA UOKOAJI UNAENDELEA


Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mbunge,Mh Mbatia muda mfupi mara baada ya kufika na kujionea hali halisi ya jengo la Ghorofa lililoporomoka mapema leo asubuhi na kupelekea watu wawili kupoteza maisha na wengine 17 kujeruhiwa vibaya.,aidha shughuli za ukoaji zinaendelea kwani inadaiwa kuna watu wengi zaidi wamefunikwa na jengo hilo.

Monday 25 March 2013

MSANII WA FILAMU KAJALA MASANJA AACHILIWA HURU LEO!

Leo ndio siku hukumu ya kesi iliyokuwa ikimkabili muigizaji Kajala iliposomwa.Katika kesi hiyo Kajala alihukumiwa miaka nane jela au kulipa faini ya milioni 13.Hivi ninavyoandika Kajala yupo nje baada ya pesa hizo kutolewa na muigizaji mwenzake Wema Sepetu.
 
Katika kesi hiyo ambayo Kajala hakuwahi kupata dhamana alikuwa ndani muda wote.Machi 15, mwaka jana Kajala na aliyekuwa mumewe walifikishwa mahakamani wakikabiliwa na kosa la utakatishaji fedha haramu ambapo kwa mujibu wa sheria kosa hilo halina dhamana.
 
Washtakiwa hao walikuwakabiliwa na makosa matatu, kosa la kwanza ni la kula njama ambapo washtakiwa wote kwa pamoja walitenda kosa kwa kuhamisha umiliki wa nyumba iliyopo Kunduchi Salasala jijini Dar es Salaam.Shtaka la pili ni ni kwamba Aprili 14 mwaka 2010 waliamisha isivyo halali umiliki wa nyumba hiyo kinyume na kifungu cha 34(2)A(3) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ya mwaka 2007. Shitaka la tatu ni la kutakatisha fedha ambalo walilitenda Aprili 14 mwaka 2010 huku wakijua ni kinyume cha sheria.
Kajala pichani walipocheza filamu ya DEVEL KINGDOM ya Kanumba pamoja na Noah Ramsey wa Nigeria.

Habari zaidi kesho katika movie leo na Zamaradi Mketema aliyekuwepo mahakama ya kisutu wakati hukumu hiyo ikisomwa!
Pia hongera Wema Sepetu kwa kumshika mkono msichana mwenzako dada!
 
 

JAMABAZI SUGU LAUWAWA KWA KUPIGWA RISASI KWENYE HARAKATI ZA KUTEKA MAGARI MLIMA NYOKA JIJINI MBEYA

Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya  Diwani akiangalia mwili jambazi lililouwawa na kikosi cha polisi Mbeya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani akionyesaha hirizi iliyofungwa katika bunduki aliyokuwa anatumia jambazi huyo kama kinga katika matukio yake 
Hii ndiyo hirizi iliyofungwa katika bunduki aliyokuwa anatumia jamabazi huyo jamani waganga wakienyeji acheni hizo kuwadanganya watu matokeo yake ni kuongeza uhalifu nchini hakika nao tutawashughulikia kwani wamekuwa chanzo cha uhalifu nchini hayo yamesemwa na kamanda Diwani,
  ..............................................................
MTU mmoja ambaye anasadikiwa kuwa ni jambazi ameuawa kwa kupigwa risasi na Askari wa Jeshi la Polisi akiwa kwenye harakati za kuteka magari katika Eneo la Mlima Nyoka Jijini Mbeya baada ya kutokea kwa majibizano ya kurushiana risasi.
 
Jambazi huyo ni miongoni mwa watu waliokuwa wakitafutwa na Jeshi la Polisi Mkoani hapa akituhumiwa kuhusika na mauaji ya Askari Polisi mwenye namba G 68 PC Jafari yaliyotokea  Februari 6, Mwaka huu  katika eneo la Matundasi Wilayani Chunya.
  
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani amethibitisha kutokea kwa tukio hilo katika Mkutano alioufanya na waandishi wa Habari Ofisini kwake ambapo alisema tukio hilo lilitokea  jana majira ya Saa 10(kumi) Alfajiri usiku wa kuamkia Machi 27, Mwaka huu.
  
Kamanda Diwani alisema kabla ya tukio majambazi wapatao wanne  tayari walikuwa wameweka mawe barabarani kwa nia ya kuteka magari ili wafanye uporaji katika eneo hilo la Mlima Nyoka ambalo limekuwa na matukio kadhaa ya watu kuporwa mali zao.
  
Alisema Jeshi la polisi baada ya kupata habari za kutegwa mawe, askari walifika kwa wakati kwa kuwa polisi walikuwa jirani na eneo hilo na kuweka mtego kwa kuwa majambazi hawakuwa wameonekana kwa wakati ule.
  
Aliongeza kuwa baada ya muda majambazi walipoona taa za gari walijitokeza tayari kushambulia lakini kabla ya hapo polisi walitoa amri ya kujisalimisha kinyume chake wakaanza kupiga risasi ovyo ndipo mashambulizi ya polisi yakafanywa.
  
Diwani alisema katika mapambano hayo alijeruhiwa jambazi mmoja kwa risasi kiunoni na ubavuni kulia na wengine watatu walifanikiwa kutoroka ambapo Marehemu alipowahishwa hospitali kwa matibabu daktari alibaini kuwa amekwisha fariki.
  
Alisema  jambazi huyo alikutwa na silaha moja SMG yenye namba  AB huku namba  nyingine zikiwa zimefutwa na magazine yake ikiwa na risasi ishirini na mbili (22) pamoja na mapanga mawili([2).
  
Aliongeza kuwa baada ya  Marehemu kufanyiwa upekuzi maungoni mwake jambazi huyo alikutwa na kitambulisho cha mkazi chenye namba B.0010453 chenye jina la Emanuel Blasius Mdendemi aliyezaliwa mwaka 1984 eneo la Matamba wilayani Makete Mkoa wa Iringa makazi yake ni Uwemba Mkoani Njombe.
  
“Jambazi huyu amebainika kuwa ni miongoni mwa majambazi waliokuwa kwenye mtandao wa majambazi uliokamatwa hivi karibuni kuhusiana na matukio waliyofanya Mikoa mbalimbali ikiwemo Mbeya,Njombe na Iringa.aidha amebainika kushiriki katika tukio la mauaji ya askari polisi PC Jafari wa kituo cha Mkwajuni – Chunya tarehe 06.02.2013.” Alisema Kamanda Diwani.
  
Aliongeza kuwa  ufuatiliaji wa majambazi waliotoroka unaendelea kufanywa ambapo pia  anatoa wito kwa yeyote mwenye taarifa za wahalifu hao azitoe bila kuchelewa kwa jeshi la polisi ili zifanyiwe kazi.

Pia  amewatahadhalisha majambazi na wahalifu wa makosa yeyote kuachana na uhalifu kwa kuwa ni biashara isiyo na faida badala yake wafanye shughuli halali kupata maendeleo ambazo fursa zake ni nyingi. 
 
Picha na  habari kwa hisani ya mbeyayetu.blogspot.com

Picha za matukio ya Kikao cha Baraza la wafanyakazi kinachoendelea kwenye ukumbi wa baraza la Maaskofu kurasini (TEC)


Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaundentia Kabaka (Mb) akifungua Baraza la Wafanyakazi wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), mapema leo 25/03/2013, katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu Kurasini (TEC) jijini Dar es Salaam
 
 Baadhi ya Wafanyakazi wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa kazi (OSHA), wakimsikiliza kwa makini Mgeni rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaundentia Kabaka (Mb)  wakati wa ufunguzi wa Baraza la wafanyakazi  katika ukumbi wa Baraza la Maaskofu Kurasini (TEC) jijini Dar es Salaam

Washiriki wa Baraza la Wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Waziri wa Kazi na Ajira Mh. Gaundentia Kabaka (Mb)

Habari zote na Afisa Uhusiano OSHA

Sunday 24 March 2013

MWENDESHA PIKIPIKI AUAWA KWA KUPIGWA RISASI NA POLISI......WANANCHI WAPANDWA NA HASIRA NA KUMUUA ASKARI HUYO

 Wananchi wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamemwua askari mmoja na kumjeruhi mwingine kwa kutumia mawe, baada ya askari hao waliokuwa doria, kumwua kwa kumpiga risasi mwendesha pikipiki (bodaboda).

Askari Polisi, PC Yohana namba 7771 alipoteza uhai katika eneo la Ngwinde kutokana na waendesha pikipiki hao kushikwa na hasira za kuuawa kwa mwenzao aliyetambulika kwa jina la Makisio Ngonyani (27), mkazi wa kijiji hicho, na hivyo kuamua kupiza kisasi.

Akizungumza na kipindi cha Radio One Stereo Nipashe, Kamanda wa Polisi mkoani Ruvuma, Deusdedith Nsimeki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo jana majira ya saa 8 mchana na kusema kuwa askari polisi wakiwa katika sare zao, walikuwa wamemfuatilia mwendesha pikipiki aliyekuwa amevunja sheria kwa kubeba abiria wawili na aliposimamishwa alikaidi.
 Baada ya kumkamata ndipo iliyopotokea purukushani ambapo risasi iliyofyatuliwa na askari ilimjeruhi mtu mmoja kidoleni kabla ya kumpata marehemu kwenye paji la uso, na kusababisha kifo chake papo.

Kamanda Nsimeki amesema, baada ya kuona hivyo, wananchi walichukua miti mikavu na mawe na kuanza kumshambulia PC Yohana na kusababisha kifo chake.

Askari aliyejeruhiwa, Konstebo Venance Kamugisha yupo katika hospitali ya Songea Mjini, kwa matibabu ya majeraha aliyoyapata kichwani na kusababisha kupoteza damu (bleeding excessively).

Kamanda Nsimeki amesema jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi ili kupata ripoti kamili.

Rais wa Jamuhuri ya watu wa China Xi Jinping kuanza ziara ya kihistoria nchini leo.

Na Eeuteri Mangi na Hussein Makame – Maelezo.
Rais wa Jamuhuri ya watu wa China Xi Jinping (pichani) anataraija kuanza ziara ya kihistoria nchini tangu kuapishwa  kwake kuitumikia  nchi hiyo ambapo katika ziara hiyo atasaini mikataba 17 ya ushirikiano wa  kiuchumi kati ya Serikali za Tanzania na nchi hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa kimataifa Bernard Membe alisema kuwa  ziara hiyo ni ya kwanza barani Afrika  kwa Rais huyo mpya wa China baada ya kuchaguliwa kuliongoza taifa hilo Machi 14 mwaka huu.
Lengo la ziara hiyo ambayo itaanza tarehe 24 hadi 25 Machi mwaka huu ni kukuza uwekezaji  na biashara baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Baadhi ya Mikataba hiyo itahusiana na uboreshaji wa sekta ya viwanda, kilimo hasa cha tumbaku ikiwemo kuwatafutia soko wakulima kutoka mikoa ya Tabora na Ruvuma ili waweze kuuza zao hilo katika soko la China.
Waziri Membe alisema kuwa; “Mikataba mingine ni ya kulipatia Shirika la Utangazaji Tanzania zana za kufanyia kazi na kuandaa mazingira ya ujenzi wa bandari ya Bagamoyo itakayounganishwa na reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA), reli ya kati na barabara”.  
Rais Xi Jinping pia atazindua na kukabidhi rasmi kituo cha Mikutano cha  Kimataifa cha Mwalimu Julius Nyerere  chenye ghorofa tatu na kumbi nne za mikutano  zenye uwezo  kupokea washiriki zaidi ya 1800 kilichogharimu dola za kimarekani milioni 29.7 zilizotolewa na Serikali ya China kwa lengo la kumuenzi Mwalimu Nyerere.
Waziri huyo alisema kuwa baada ya kufika nchini Rais Xi Jinping atazungumza na mwenyeji wake Rais Dk. Jakaya Kikwete pamoja na Viongozi Waandamizi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na baadaye atahudhuria dhifa ya kitaifa Ikulu Jijini Dar es salaam.
Siku ya pili ya ziara yake Rais Jinping  atazungumza rasmi na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Ali Mohamed Shein pamoja na ujumbe wa viongozi waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Waziri Membe aliongeza kuwa Rais Jinping atatoa hotuba maalumu kwa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla na  kuzungumzia sera ya Serikali mpya ya China kwa bara la Afrika ambayo itahudhuriwa na watu kutoka kada mbalimbali ikiwemo Viongozi na Maafisa Waandamizi wa Serikali, Wahadhiri wa Vyuo Vikuu,Wabunge, Viongozi wa Dini na Asasi za Kiraia na Wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.
“Hotuba hiyo ya Rais wa China ataitoa kwa lugha ya Kichina na kutafsiriwa  kwa lugha ya Kiingereza na Kiswahili ili iweze kuifika dunia nzima, hivyo tunaviomba vyombo vya habari nchini vichukue fursa hiyo kuwa vya kwanza kuutangazia Ulimwengu” alisema Waziri Membe.
Ziara hiyo ya Rais wa Jamhuri ya Watu wa China  ni muendelezo wa uhusiano mzuri kati ya nchi hiyo na Tanzania ulioasisiwa na viongozi  wa mataifa hayo mawili, yaani Mao Zedong wa China na  Mwalimu Julius Nyerere wa Tanzania.
Rais Jinping ataondoka nchini Machi 25 saa 10:40 jioni kuelekea nchini Afrika Kusini kuhudhuria mkutano wa tano wa Wakuu wa Nchi zinazokuwa kwa kasi kiuchumi ambazo ni Brazil, Urusi, India, China na Afrika ya Kusini (BRICS).

TAIFA STARS YAWAZABA LIONS OF THE ATLAS

Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wamewainua watanzania kwa kumzaba Morocco mabao 3-1 katika mechi ya kuwania kufuzu kucheza Kombe la Dunia.

Mabao ya Taifa Stars yametupiwa na Thomas Ulimwengu katika dakika ya 46 na Mbwana Samatta alizifumania nyavu katika dakika za 67 na 80.

Bao pekee la Lions of The Atlas limefungwa katika dakika ya 90 ya mchezo huo ambao umechezwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Pia katika mechi hiyo mchezaji wa Morocco Abderrahim Chakir alionyeshwa kadi nyekundu kufuatia kucheza vibaya.

Kwa matokeo hayo Stars inaendelea kushika nafasi ya pili ikiwa na alama 6 kutokana na Ivory Coast jana kumnyuka Gambia mabao 3-0 na kuwa na pointi 7 ikipisha alama moja tu na tembo hao wa Afrika.

Thursday 21 March 2013

ZIARA YA RAIS DK. SHEIN MKOANI PEMBA


DSC_0015
Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,akipokea Taarifa ya ujenzi wa kituo cha Afya
Tasini  Kiwani kutoka kwa Mwalimu Abdalla Juma Mustafa, baada ya
kukagua maendeleo ya Ujenzi wa kituo hicho,akiwa katika ziara ya
Wilaya ya Mkoani Pemba jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
DSC_0011Wananchi wa Tasini  Kiwani wakimsikiliza Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipofika
kuwasalimia baada ya  kukagua maendeleo ya Ujenzi wa barabara ya
vijiji hivyo  akiwa katika ziara ya Wilaya ya Mkoani Pemba jana.[Picha
DSC_0028 Baadhi ya wanafunzi na Wazee wa wakimsikiliza Rais wa wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed
Shein,alipokuwa akizungumza nao alipokagua ujenzi wa kituocha Afya na
barabara ya Tasini Kiwani ,akiwa katika ziara ya Wilaya ya Mkoani
Pemba jana.[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.] DSC_0030Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Dk.Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto) na Viongozi wengine wakiitikia
dua baada ya kukamilika kwa harambeee aliyoiitisha kuchangia ujenzi wa
Kituocha Afya Tasini Kiwani Wilaya ya Mkoani Pemba,akiwa katika ziara
ya kikazi ndani ya Mkoa huo. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
DSC_0039Rais wa wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) alipofika kukagua wagonjwa
akianza na Mzee Hassan Kombo,aliyepata ajali ya vespa akiwa katika
Hospitali ya Mkoani Pemba,katika ziara ya   kikazi ndani ya Mkoa huo.
[Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]
DSC_0043Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein, alipofika kukagua wagonjwa
katika Hospitali ya Abdalla Mzee,Mkoani Pemba,pichani Dk.
Shein,akimuangalia Mtoto Husna Mohamed Kombo,(kichanga) akiwa na Mama
yake  Riziki Haji,mtoto huyo anasumbuliwa na kitovu,Rais akiwa
kisiwani Pemba kwa Ziara ya kikazi ndani ya Mkoa wa Kusini . [Picha na
Ramadhan Othman,Ikulu.]

DSC_0095 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(wa nne kushoto) akipatra maelezo
Kutoka kwa Katibu Mkuu Wizara ya nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Salum Maulid, (Kibanzi) alipotembelea matengenezo
makubwa ya Ikulu Ndogo ya Mkoani Pemba,alipokuwa katika ziara ya Mkoa
wa Kusini Pemba jana. [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

Thursday 14 March 2013

TUJIJENGEE MAZINGIRA YA KUPIMA AFYA ZETU


Siku ya mmiliki wa blog ya demashonews alipochukua jukumu la kupima afya yake kwa hilayali katika kituo cha afya kilichopo Madaba songea vijijini Mkoani Ruvuma.
Ni uso wenye furaha tele baada ya kupewa majibu yake " wito wangu kwa watanzania wenzangu kuwa na  tabia ya kupima afya zetu mara kwa mara tusingojee pale unapokuwa na tatizo ndipo ukapime afya yako" hayo ndio maneno aliyoyasema mmiliki wa blog ya demashonews baada ya kupima afya .

CHINA YAITABIRIA TANZANIA KUPIGA HATUA



1. KINANA NA UJUMBE WAKE KWENYE MNARA WA PILI DUNIANI KWA UREFUaMtumishi katika mnara wa Canton, mrefu kuliko yote nchini China na watatu duniani kwa urefu, Sarah Xie, akimuonyesha mandhari ya jiji la Guangzhou, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, wakati Kinana na ujumbe wake walipopanda hadi mwisho mnara huo wenye urefu wa zaidi ya futi 100, Machi 13, 2013. Wengine Kulia ni Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na Katibu Mkuu wa UVCCM, Martine shigella. Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo). 3. KINANA NA UJUMBE WAKE NDANI YA MNARAaKatibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakitazama maumbo ya mandhari ya mji wa Guanzhou, China, yaliyopo ndani ya mnara wa Cnton wenye urefu wa zaidi ya mita 100, walipotembelea mnara huo, Machi 13, 2013.  Kinana na ujumbe wake wapo nchini kwa ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo).
10. DK. MIGIRO NA MAOFISA WA IDARA YA MAMBO YA NJE WA DONGGUANSABINA LIU (L) NA SARAH XIEaKatibu wa NEC, Ushirikiano wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro (kushoto) na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa mjini Magharibi, Yussuf Mohamed Yusuf wakitaza bidhaa zinazouzwa kwenye kilele Mnara wa Canton ambao ni mrefu kuliko yote nchini China ukiwa na urefu wa zaidi ya mita 100, mjini Guangzhou, China. Dk. Asha-Rose Migiro na Yusuf ni miongoni mwa viongozi walioambatana na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana katika ziara ya siku kumi ya kimafunzo kwa mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC). (Picha na Bashir Nkoromo).
13. KINANA NA MIGIRO WAKIWA NA VIONGOZI WA CHAMA CHA WA-TZ WAISHIO CHINA. (L) DAVID CHAMALA (KTB), JOHN LUHEMBA (MKT)-L, ABRAHAM MERISHANI MAKAMU MKT NA ABUBAKAR MWINYI KATB MSAIDIZIaKatibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwa katika picha ya pamoja na viongozi na wanachama wa Jumuia ya watanzania waishio nchini China

NA BASHIR NKOROMO, DONGGUAN,CHINA

CHAMA Cha Kikomunisti cha China (CPC) kimeeleza matumaini yake kwamba upo uwezekano wa Tanzania kupiga hatua kubwa kichumi kama inajikita kwa dhati katika kuzitumia rasilimali ilizonazo ikiwemo ardhi.
Hayo yalisemwa Machi 13, 2013 na Kamishna wa Maadili na nidhamu wa Chama Cha Kikomunisti cha China (CPC), jimbo la Donguan, China,  Cuo Jian, wakati akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na ujumbe wake, katika hoteli ya Exhibition Internation mjini hapa.
Jian ambaye pia ni Meya wa jiji la Donguan, alisema, Tanzania kama zilivyo nchi kadhaa za Afrika, inaweza kupiga hatua kiuchumi ikiwekeza juhudi zake katika kuzitumia rasilimali ilizonazo kwa kuwa rasilimali ndiyo msingi wa kwanza katika kuinua uchumi wa nchi yoyote.
Alisema, anatambuwa kwamba Tanzania ni moja ya nchi za Afrika zenye ardhi kubwa, hivyo haina budi juhudi zake za kuinua uchumi kuzielekeza katika rasilimali hiyo ikiitumia kwa kilimo cha kisasa, kujenga viwanda na vitegauchumi mbalimbali ambavyo vitachochea kukua haraka kwa uchumi.
“Hata hivyo nawapongeza Tanzania, kwa hatua mliyofikia sasa katika kukuza uchumi, asilimia sita ya GDP, inaridhisha, la msingi serikali  kuongeza juhudi na kuwahamasisha wananchi kushiriki katika juhudi hizo”, alisema, Jian.
Akijibu swali na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu, ambaye yupo kwenye msafara wa Kinana katika ziara hiyo, Titus Kamani aliyetaka kujua ni nini hasa China ilifanya hadi kuufanya uchumi wake ukue haraka na kuwa nchi ya pili dunia kwa maendeleo, Jian alisema, China imefikia mafanikio hayo kutokana na kuamua kuwekeza kwa nguvu zake zote kwenye rasilimali ya ardhi.
“Zipo njia nyingi za kuweza kuinua uchumi wa  nchi yoyote, juhudi hizo baadhi zinafanana na nyingine ni tofauti kutokana na nchi na nchi, lakini sisi (Wachina) tulifahamu kwamba tuna ardhi kubwa sana, hivyo tukaamua kuimua rasilimali hii kwa kila namna iliyo bora. Licha ya eneo kuwa kubwa lakini tumehakikisha hakuna eneo linaloachwa bila faida”, alisema.
Kwa upande wake Kinana aliupongeza uongozi wa China chini ya chama cha CPC na wananchi wa nchi hiyo kwa kuweza kufanikisha kuinua uchumi wa nchi hiyo kwa kiwango kibwa cha sasa.
“Bila shaka ni uchapakazi usio na kikomo na wakujituma sana kwa pamoja kati ya serikali na wananchi ndiyo maana mmefanikiwa hivi, napenda kuchua fursa hii niwapongeze kwa dhati kwa mafanikio haya, nasi kama nchi rafiki tunapata kiu kubwa kuhakikisha tunafika mlipo au angalau kuwakaribia”, alisema Kinana.
Kinana yupo nchini China akiambatana na ujumbe wa viongozi na maofisa wa Chama kwa ajili ya ziara ya mafunzo, katika nyanja mbalimbali za kiuchumi na kisiasa, na pia kudumisha urafiki wa kindugu wa siku nyingi kati ya Chama Cha Mapinduzi na Chama Cha Kikomunisti cha nchi hiyo.
Katika ziara hiyo Kinana amefuatana na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Zanzibar), Vuai Ali Vuai, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Khadija Aboud, Katibu wa NEC, Siasa na Uhuaisno wa Kimataifa, Dk. Asha-Rose Migiro, Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM, Martine Shigela, Katibu Mkuu wa Jumuia ya Wazazi, Khamis Suleiman Dadi na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mjini Magharibi Mohammed Yusuf Mohamed.
Wengine ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa,  Jesca Msambatavangu, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Simiyu Titus Kamani, Katibu wa CCM mkoa wa Mbeya Maganga Sengelema na maofisa wa Chama. ziara hiyo
Kinana anafanya ziara  hiyo kutokana na mwaliko wa Chama Cha Kikomunisti cha China, na anafanya ziara hiyo ikiwa ni ya kwanza kuifanya nje ya nchi, tangu alipoteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM, Oktoba mwaka jana mjini Dodoma
Chanzo cha habari http://www.fullshangweblog.com

Monday 11 March 2013

MSAADA WAKO UNAHITAJIKA ILIKUWEZA KUOKOA UHAI WA MTOTO SIMON MLOPE



Hivi ndivyo hali ya mtoto Simon Mlope ilivo kwa sasa
 Mtoto Simon Mlope akiwa na mama yake ambaye anaitwa Amina Ally
Angalia Video ya  mtoto Simoni Mlope akiwa na Mama yake. 
 

Mtoto simon Mlope mwenye umri wa miaka 11 mkazi wa eneo la mahenge katika manispaa ya songea mkoani Ruvuma amelazimika kukatisha masomo yake ya shule ya msingi akiwa darasa kwanza  kutokana na mototo huyo kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo .
Awali tulitoa habari za mtoto huyu akiomba msaada lakini hadi sasa bado hajapata msaada wowote ule wa kuweza kuokoa maisha yake. Nahivi sasa hali ya mtoto huyu inazidi kuwa mbaya kiafya .

 Mtoto simon Mlope alikubwa na ugonjwa  moyo  tangu mwaka 2001 mara baada ya kuzaliwa na kugundulika kuwa  moyo wake una tundu hali ambayo inasababisha  kuvuta pumzi kwa shida.
Mama wa mototo  simon mlope anayeitwa AMINA ALLY  anawaomba watanzania kumsaidia mtoto  wake fedha za matibabu Baada ya kuambiwa na madaktari kuwa simon anatakiwa kwenda nchini  india kutibiwa,baada ya kupata rufaa kutoka muhimbili mwaka 2006  huku familia yake ikiwa haina uwezo kabisa.

Majirani wa familia ya simon nao wanasema kuwa mototo simon anahitaji msaada wa haraka kwa kuwa hali yake sio nzuri na kuwaomba watanzania wamsaidie.
Kinachosikitisha zaidi baba wa mtoto huyo  anayejulikana kwa jina la SIMON MLOPE  ameondoka nyumbani hapo tangu mwaka 2011 na hajulikani aliko kwa sasa, ingawa mwanzoni alisema yuko nchini Msumbiji.
Kwa anayeguswa na tatizo hili na anataka kumsaidia  SIMONI MLOPE  atumie simu namba  0752732290
Picha na habari kwa hisani ya http://demashonews.blogspot.com

Friday 8 March 2013

MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU ATOA ONYO KWA WALE WANAOUZA MAZAO YAO BILA KUSHIRIKISHA WAKE ZAO.



Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwangu akizungumza katika siku ya wanawake duniani

Mkuu wa Wialaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti akitambusha viongozi aliofatana nao

Mwenyekiti wa kamati ya wafanyakazi wanawake wa chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa (TALGWU) Taifa dokta ANGELINA SANIKE akijitambulisha .
 Kikundi cha cha akina mama kikitoa burudani katika maadhimisho hayo
 Wanafunzi wa shule ya msingi wakicheza kiduku ya asili kwa kupigiwa ngoma za asili
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akitoa zawadi ya sale ya shule, madaftali na sabuni kwa mtoto yatima ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akitoa zawadi ya sale ya shule, madaftali na sabuni kwa mtoto yatima ambaye ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari

 Viongozi mbalimbali toka serikali wakifatilia kwa umakini kilichokuwa kinaenelea uwanjani
 Kikundi cha ngoma ya asili kikitoa burudani ya (Ngoma ya Lizombe)
............................................................


Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia  iliyiadhimishwa kimkoa  katika kijiji cha Lusonga Wilaya ya Songea.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma SAIDI MWAMBUNGU amekemea vikali vitendo vya kikatili vinavyofanywa dhidi ya wanawake katika mkoa wa Ruvuma.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha lusonga wilaya ya Songea hapo jana MWAMBUNGU amesema ni marufuku wanaume kuuza mazao yao bila kushirikisha wake zao. Na kwawale  wanaotenda hivo watachukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa ni moja wapo ya ukatili dhidi ya wanawakePia  amesema serikali inafanya juhudi ya kutokomeza vitendo vya kikatili vinavyofanywa dhidi ya wanawake.

Akisoma risala katika maadhimsho ya siku ya wanawake iliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Lusonga wilaya ya Songea mkoani Ruvuma afisa maendeleo ya jamii wa wilaya WENISARIA SWAI amesema kuwa katika mkoa wa Ruvuma wananawake ndio wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula na biashara lakini hawashirikishwi katika kutoa maamuzi.

Amesema wanawake wengi katika familia wananyimwahaki ya kushirikikatika kutoa maamuziya mgawanyo wa mapato yanayopatikana ingawa wao ndio wazalishaji na watendaji kazi wakubwa.Aidha shughuli nyingi zinazofanywa na wanaake hazina ujira hali inayosababisha ndoa kukosa malezi mema hatimaye watoto na vijana kuondoka nyumbani na kujiingiza katika makundi ya ombaomba mitani.

Naye mwenyekiti wa kamati ya wafanyakazi wanawake wa chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa (talgwu) taifa dokta ANGELINA SANIKE ametoa wito kwa jamii kuelimsha watoto kike ili kuondokana na mfumo dume .

MKURUGENZI WA MAFUNZO YA UFUNDI JESHI LA KUJENGA TAIFA KANALI CHACHA WANYANCHA AFUNGA MAFUNZO YA UZALISHAJI UMEME KWA KUTUMIA NISHATI ITOKANAYO NA BAYOGESI (JKT MLALE)


Mkurugenzi wa mafunzo ya ufundi Jeshi la kujenga Taifa Kanali Chacha Muninka Wanyancha

Injinia wa Wakala wa Nishati Vijijini Enocent Nyemoakitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa mafunzo ya ufundi Jeshi la kujenga Taifa Kanali Chacha Muninka Wanyancha kuhusu mtambo utakao wekwa katika shimo lililochimbwa kwa ajili ya kuweka mtambo.
 Mkurugenzi wa mafunzo ya ufundi Jeshi la kujenga Taifa Kanali Chacha Muninka Wanyancha akisikiliza melezo toka kwa mkuu wa Kambi ya JKT Mlale

..................................................................


Katika hafla ya kufunga mafunzo hayo Kanali Chacha Wanyancha  amewataka wahitimu watambue kuwa wanalo jukumu kubwa mbele yao baada ya kupata mafunzo ya uzalishaji umeme kwa kutumia nishati jadidifu itokanayo na Bayogesi kwa kuwa wao ndio watakaokuwa chachu ya uhamasishaji wa matumizi bora na sahihi ya nishati jadidifu katika  maeneo yao baada ya kuhitimu mafunzo haya. 

“Kufanya kwa mafunzo haya kutawezesha kufikia malengo ya Milenia, MKUKUTA na sera ya Taifa ya Nishati ambayo yanalenga katika upatikanaji wa nishati bora kwa lengo la kukuza uzalishaji mali na kuendeleza huduma za  jamii, pia  kutokana na mafunzo waliopata yatasaidia kupatikana kwa huduma bora za nishati mbadala na endelevu kutachochea kuchangia katika kupunguza  umaskini na uharibifu wa mazingira ambayo kwa sasa ni tatizo kubwa.

Katka  hutuba yake  Kanali Chacha Muninka amezitaja changamoto mbalimbali zinazowakabili wadau kwenye uendeshaji wa vyanzo vya nishati vijijini, kamavile ukosefu wa mitaji, uwezo mdogo wa kiutaalamu  na wa kiufundi, mabadiliko ya hali ya hewa  na athari za mazingira pia kutojua fursa zilizopo katika uwezeshwaji wa kuanzisha miradi ya aina hii. Changamoto hizi zinaweza  kumalizika iwapo kutakuwa na  ushirikiano wa karibu na wadau , wakala wa Nishati Vijijini na Taasisi za ndani na nje zinazojishirikisha  na nishati vijijini na masuala ya mazingira.

Naye Inocent Msua  amesema kuwa wakala wa Nishati vijijini wanatoa ruzuku kwa waendelezaji wa miradi ya nishati vijiji kama sehemu yake ya kuchangia  kukabiliana  na tatizo la mitaji. Wakala  hawa wa Nishati Vijijini wamekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha mabenki na taasisi nyingine za fedha za ndani na nje ya nchi kutoa mikopo yenye riba na masharti nafuu kwa waendelezaji wa miradi ya nishati vijijini hapa Tanzania.
Pia ameongezea kuwa tayari mpango huu kwa sasa unatekelezwa na benki za TIB,CRDB,NBC,NMB,TWIGA BANCORP na AZANIA. 
 

Thursday 7 March 2013

SAI-BABA EXPLESS LA GONGA NA KUUA HAPO HAPO- SONGEA


 TUNAOMBA RADHI KUNAPICHA SINZURI KWA KUANGALIA ILA IMETUBIDI TUWEKE KWA AJILI YA KUONYESHA UKWELI WA JALI JINSI ILIVYOTOKEA

 Hili ndio Bus lililogonga  lenye namba za usajili T 690 BUW

Hawa ni abilia wakieleza namna ya ajali ilivotokea leo maeneo ya kwa Mburushi
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Deusdedit Nsimeki alie vua kofia akiwa katika eneo la tukio maeneo ya kwa Mburushi
Dereva wa Bus la Sai - Baba Expless  Bw. Robison Sanke (57
 Hii ndio pikipiki ya marehemu  Steven Adam (62) yenye namba za usajili  T 618 ATX
 Umati wa wasafiri wakiwemo wapita njia wakiangalia ajali hiyo mbayailiyotokea leo majira ya saa moja asubuhi, TUNAOMBA RADHI KWA PICHA ZINAZOFUATA HAPO CHINI KWANI ZINATISHA,
 Hivi ndivyo ilivyotokea ajali hiyo leo majira ya saa moja maeneo ya kwa Mburushi 
Mwili wa Steven Adam ukiwa umelala chini baada ya ajali

Bus la Kampuni ya SAI – BABA EXPLESS lenye namba ya usajili  T 690 BUW likiwa safarini kuelekea Dar Es Salaam likitokea Songea limepata ajali leo majira ya saa moja na nusu asubuhi maeneo ya kwa Mburushi mjini songea.
Bus hilo limemgonga Dereva wa pikipiki (yeboyebo) ambaya ni mkazi wa Liumbu Mletele aliejulikana kwa jina la Bw. Steven Adam (62) mfanya biashara ya maziwa .
 Marehem Steven alikuwa akielekea mjini kupeleka mazima yake kwa wateja ndipo alipotwa na mahuti hayo. Kwa maelezo ya wasafiri wamesema mwenye makosa ni dereva Pikipiki ambaye hakuwa makini barabari kwa kuendesha vibaya na kwamwendo kasi pasipo kuzingatia sheria za barabarani.

TUPE MAONI YAKO