Thursday 30 October 2014

UPEPO MWINGINE BWANA NOUMA

UPEPO mkali uliozuka katika Kijiji cha Molandi kilichpo katika Kata ya marimba Wilayani Tunduru Mkoani Ruvuma Umeezua Nyumba 10 na kuziacha familia hizo zikiwa hazina makazi.

Aidha taarifa za awali zinaeleza kuwa katika tukio hilo upepo huo umeezua nyuma 7 za bati na nyumba 3 zilizotuku zimeezekwa kwa nyasi na umesababisha hasara ya kumla ya Shiringi Milioni 11.925,000.
Taarifa za tukio hilo zinaeleza kuwa zuruba hilo liliwakumba wakazi wa Kijiji hicho Oktoba 12 mwaka huu majira ya saa 7 mchana na kuzusha taharuki kubwa kwa wakazi wa kijiji hicho.

 Taarifa hiyo inafafanua kuwa Sambamba na tukio hilo pia upepo huo ilisomba moto ambao ulisababisha ungua kwa nyasi zilizotuka kuezekea baadhi ya nyumba pamoja na kuunguza uwanja wa timu ya Kijiji hicho ya Nyuki Fc.
Akiongea kwa njia ya simu Diwanai wa wa kata hiyo Bw. Msenga Saidi alidhibitisha kutokewa kwa tukio hilo na kuongeza kuwa kufutia tukio hilo wahanga kutoka katika kaya hizo hivi sasa wanahidhiwa katika nyumba za majirani ambao nyumba zao zilinusulika.

Bw. Msenga aliwataja wahanga wa tukio hilo kuwa ni Bw. Omary Jafari Mchali, Abdalah Said Manjolo, Abdalah Halifa Limbanga na Mohammed Omary Mangwila.

 Kwamujibu wa diwani huyo wahanga wengine ni Said Omari Yazidu, Ommari kazembe Nangwale,Mohammed Kazembe Nangwale, Mohammed Makunganya Mohhammed Juma wandale 

 Nae mwenyekiti wa kamati ya maafa,ulinzi na usalama Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Chande Nalicho pamoja na mambo mengine alisema kuwa baad ay atukio hilo kamati yake iliwatembelea wahanga hao na kuwapa pole.
Alisema wakiwa katika eneo hilo pia walizungumza na wahanga hao pamoja na kuwapatia ushauri wa kufuata hatua za ujenzi imara wa nyumba zao pamoja kupanda miti ya kujikinga ma majanga ya aina hiyo.
Mwisho

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO