Monday 18 February 2013

Mwadhama Kardinal Pengo azunguzia kifo cha Padri Zanzibar, wauaji waacha ujumbe baada ya mauaji.



Moja ya vipeperushi vilivyokamatwa mjini Zanzibar alipopigwa risasi Padri wa Kanisa Mpendae alichokionyesha Mwadhama kardinali Polycap Pengo alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo
Pengo asikitishwa na tukio la kuuwa kwa Padri Mushi lililotokea Mjini Zanzibar na kuwaasa wakristu kutolipiza kisasi maana kufanya hivyo yanaweza kutokea machafuko makubwa zaidi, la msingi alilosisitiza ni kwamba wale wanaopaswa kulinda usalama waangalie sana tunakoelekea siyo kuzuri ukilinganisha na matukio yanayoendelea
 
Pengo aliyekuwa anazungumza huku akiwa mwenye hudhuni hakuzungumza kwa muda mwingi sana na baada ya hapo alisema nawashukuru sana waandishi hayo ndiyo niliyokuwa nayo na kuongeza kuwa leo sitajibu maswali yoyote asante sana na kuondoka ukumbini

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO