Wednesday 11 September 2013

SOMA TANGAZO KUTOKA WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII:NAFASI ZA AJIRA KWA MADAKTARI, MADAKTARI WA MENO, TABIBU, TABIBU WASAIDIZI NA WATAALAMU WA MAABARA

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, inawatangazia Wahitimu wa taaluma zilizotajwa hapo juu kuwa zipo nafasi za kazi katika Mikoa na Halmashauri zote nchini isipokuwa Mkoa wa Dar es Salaam na Halmashauri zake.

Waombaji wanatakiwa kuambatanisha nyaraka zifuatazo katika maombi yao:-

  1. Vyeti vya Elimu ya Sekondari.
  2. Cheti cha Kuhitimu mafunzo ya taaluma husika.
  3. Kwa wale wanaotakiwa  Kwa mujibu wa sheria  kufanya mafunzo kwa vitendo, wawasilishe cheti cha kuhitimu mafunzo hayo.
Mwisho wa kupokea maombi ni wiki mbili kuanzia tarehe ya tangazo hili kutoka. Aidha, juu ya bahasha iandikwe nafasi inayoombwa.

Majina ya watakaopangiwa vituo vya kazi yatatangazwa kwenye tovuti ya Wizara www.moh.go.tz

Barua zote zipitie Posta. Aidha, barua zitakazoletwa kwa mkono hazitopokelewa
Maombi hayo yatumwe kwenye anuani ifuatayo:- 

KATIBU MKUU,
WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII,
S.L.P. 9083,
DAR ES SALAAM.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO