Wednesday 6 March 2013

Wakazi wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamelalamikia uharibifu wa mazao mahindi na mpunga unaofanywa na mifugo.

Wakazi wa wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma wamelalamikia uharibifu mkubwa wa mazao yao ya mahindi na mpunga unaofanywa na mifugo aina ya ng'ombe walioingizwa wilayni humo kinyume na sheria.

Akizungumza kwa niaba ya wakazi wa wilaya ya Tunduru mkuu wa wilaya hiyo ABDALLAH LUTAVI amesema ng'ombe hao wameenea katika maeneo mabalimbali ya vijiji na kushambulia mazao ya wakulima.


Amesema serikali imeanza kuchukua hatua dhidi ya wale wanaolisha mifugo yao katika mashamba ya watu na kuomba kikao hicho kiweke mkakati wa haraka kuzuia uingizwaji wa mifugo hiyo ili kujiepusha na njaa inayoweza kutokea kutokana na mazao kushambuliwa na mifugo hiyo.


Mkuu wa wilaya ya Namtumbo ABDALLAH LUTAVI alikuwa akizungumza katika kikao cha ushauri cha mkoa wa Ruvuma kilichofanyika katika manispaa ya Songea.


Naye mbunge wa Jimbo la Namtumbo Mheshimiwa vita kawawa amesema ng!ombe hao wakiachwa kwa kipindi cha mwaka mmoja tu basi wilaya hiyo itakosa kabisa mazao.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO