Friday 8 March 2013

MKUU WA MKOA WA RUVUMA SAID MWAMBUNGU ATOA ONYO KWA WALE WANAOUZA MAZAO YAO BILA KUSHIRIKISHA WAKE ZAO.



Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabit Mwangu akizungumza katika siku ya wanawake duniani

Mkuu wa Wialaya ya Songea Joseph Joseph Mkirikiti akitambusha viongozi aliofatana nao

Mwenyekiti wa kamati ya wafanyakazi wanawake wa chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa (TALGWU) Taifa dokta ANGELINA SANIKE akijitambulisha .
 Kikundi cha cha akina mama kikitoa burudani katika maadhimisho hayo
 Wanafunzi wa shule ya msingi wakicheza kiduku ya asili kwa kupigiwa ngoma za asili
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akitoa zawadi ya sale ya shule, madaftali na sabuni kwa mtoto yatima ambaye ni mwanafunzi wa shule ya msingi.
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu akitoa zawadi ya sale ya shule, madaftali na sabuni kwa mtoto yatima ambaye ni mwanafunzi wa shule ya Sekondari

 Viongozi mbalimbali toka serikali wakifatilia kwa umakini kilichokuwa kinaenelea uwanjani
 Kikundi cha ngoma ya asili kikitoa burudani ya (Ngoma ya Lizombe)
............................................................


Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Bw. Said Mwambungu katika maadhimisho ya siku ya wanawake dunia  iliyiadhimishwa kimkoa  katika kijiji cha Lusonga Wilaya ya Songea.

Mkuu wa mkoa wa Ruvuma SAIDI MWAMBUNGU amekemea vikali vitendo vya kikatili vinavyofanywa dhidi ya wanawake katika mkoa wa Ruvuma.
Akizungumza katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa katika kijiji cha lusonga wilaya ya Songea hapo jana MWAMBUNGU amesema ni marufuku wanaume kuuza mazao yao bila kushirikisha wake zao. Na kwawale  wanaotenda hivo watachukuliwa hatua za kisheria kwa kuwa ni moja wapo ya ukatili dhidi ya wanawakePia  amesema serikali inafanya juhudi ya kutokomeza vitendo vya kikatili vinavyofanywa dhidi ya wanawake.

Akisoma risala katika maadhimsho ya siku ya wanawake iliyofanyika kimkoa katika kijiji cha Lusonga wilaya ya Songea mkoani Ruvuma afisa maendeleo ya jamii wa wilaya WENISARIA SWAI amesema kuwa katika mkoa wa Ruvuma wananawake ndio wazalishaji wakubwa wa mazao ya chakula na biashara lakini hawashirikishwi katika kutoa maamuzi.

Amesema wanawake wengi katika familia wananyimwahaki ya kushirikikatika kutoa maamuziya mgawanyo wa mapato yanayopatikana ingawa wao ndio wazalishaji na watendaji kazi wakubwa.Aidha shughuli nyingi zinazofanywa na wanaake hazina ujira hali inayosababisha ndoa kukosa malezi mema hatimaye watoto na vijana kuondoka nyumbani na kujiingiza katika makundi ya ombaomba mitani.

Naye mwenyekiti wa kamati ya wafanyakazi wanawake wa chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa (talgwu) taifa dokta ANGELINA SANIKE ametoa wito kwa jamii kuelimsha watoto kike ili kuondokana na mfumo dume .

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO