Thursday 4 April 2013

Mkuu wa Wilaya ya Songea afungua kikao cha baraza la wafanya kazi wa shirika la mzinga

 Mkuu wa wilaya ya Songea Bwn:Joseph Mkirikiti

 
Mkuu wa wilaya ya Songea JOSEPH MKIRIKITI amelitaka shirika la mizinga kutumia wafanykazi wake wasomi kutengeneza ajira za vijana ambao wengi hawana mwelekeo wa maisha.
Mkuu wa wilayay ya songea amesema hayo wakati akidungua kikao cha tano cha baraza la wafanyakazi la shirika la mizinga kilichofanyika katika manispaa ya songea mkoani Ruvuma.

Joseph Mkirikiti amesema kikosi cha mizinga kina wasomi ambao wakitumika vizuri wanaweza kutumia taaluma zao kutengeneza ajira za vijana .

Awali akitoa taarifa ya ufunguzi wa kikao cha baraza la wafanyakazi wa shirika hilo, Meja jenerali CHARLES MUZANILA amesema kikao hicho ni utekelezaji wa siasa ya ushirikishwaji wa wafanyakazi mahali pa kazi kama ilivyoagizwa na tamko la hayati baba wa Taifa tamko namba 1 mwaka 1970 na sheria zingine za kazi kwa madhumuni ya kuondoa migogoro sehemu za kazi na kuongeza tija.



 Meja jeneral Chalres Munazila akisoma taarifa ya baraza la wafanyakazi wa shirika la mzinga
Meja jenerali Muzanila amesema shirika la mizinga kwa muda wa mwaka mmoja limefanikiwa kusimika mitambo mipyaya uzalishaji wa mazao ambayo ilizinduliwa  na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania mwaka jana.

kuanzisha miradi mbalimbali katika kupunguza utegemezi wa ruzuku kutoka serikalini kwa kutengeneza samani,za kisasa za maofisini na majumbani, uuzaji wa milipuko na viwashiovya kiraia kwa ajili ya wachimba madini na wapasua kokoto.


 Wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa shirika la mzinga wakiimba wimbo wa mshikamano daima kabla ya kuanza kikao.




 Wajumbe wa baraza la wafanyakazi wa shirika la mzinga wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Songea JOSEPH MKIRIKITI.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO