Thursday 15 August 2013

MSHINDI MISS ILALA KULAMBA MILIONI 1,500,000 KESHO

DSC_0134 

MREMBO atakayetwaa taji la Redds Miss Ilala 2013, linalofanyika kesho Agosti  16, ataondoka na zawadi za jumla ya Sh. Milioni 1,500,000,huku mshindi wa pili atajipatia shilingi milioni moja na wa tatu shilingi laki saba.  
Mbali na zawadi hiyo, washindi hao watatu watapata ofa ya ya miezi sita kutoka RIO gym & Spa, iliyopo Quality Center, kutumia vifaa vyote ndani ya gym hiyo ambayo gharama yake ni Milioni 900,000 kwa kila mtu.  
Sh , 400,000 zitakwenda kwa mshindi wa nne na atakayeshika nafasi ya tano yeye ataibuka na Sh 300,000. Washiriki wengine ambao hawatabahatika kuingia katika nafasi ya tano bora, wote watapewa Sh,200,000 kwa maana ya kifuta jasho. Tumelenga zawadi za fedha zaidi, hii ni kutokana na ugumu wa maandalizi kwa warembo ambao hugharamika zaidi, kiasi nasi kuona kuna kila namna ya kuwapunguzia maamivu hayo.  
Shindano hilo, linatarajiwa kuwa na burudani ya kipekee kutoka kundi zima la Tanzania House of Talent (THT) wakiongozwa na mwanadada mwenye sauti ya chiriku, Lina na Barnaba. Kundi la Wanne Star nalo litajumuika katika kuufanya usiku wa kesho kuwa wa burudani tosha kutokana na kuja kivingine kabisa katika nyimbo za asili za Afrika. Warembo watakaopanda jukwaani Julai 5 ni kutoka Kigamboni, Kurasini na Chang’ombe ambao wanawania taji linaloshikiliwa na Miss Tanzania namba tatu, Edda Sylvester walikuwa chini ya wakufunzi Suzy Mwenda na Shadya Mohamed wakati kwenye kucheza nako walikuwa na walimu wawili Super Bokilo na Charles.  
Warembo wataoapanda jukwaani hityo kesho ni 14 Diana Kato, Martha Gewe, Alice Issac, Irine Mwelelo, Clara Bayo, Natasha  
Mohamed, Doris Molel, Upendo Lema, Kabula Kibogoti, Shamim Mohamed, Kazunde Kitereja, Rehema Mpanda, Johanither Kabunga,Anna Johnson.  
Shindano hilo limedhaminiwa na kinywaji cha Redd’s, Dodoma Wine, Gazeti la Jambo Leo, Cloud’s Media, Blogu ya Wananchi (Le Mutuz), Fredito Entertainment, CXC Africa tours & Safaris, RIO Gym& Spa, Smile Internet, Delina Interprises na Kitwe General Traders. Ilala Interteinment  ndiyo inayoandaa mashindano haya, inatanguliza shukrani zake 

wadhamini wetu kwa miaka hiyo, sanjari na vyombo vyote vya habari kwa ujumla wake, kwani ndio waliofanikisha kufanikisha shughuli yetu ya kesho.
by John Bukuku 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO