Wednesday 19 December 2012

PINDA AKAGUA SHAMBA LA RC WA KATAVI

 Waziri Mkuu Mizengo akipalilia mahindi ili kumwonyesha Bi. Yusta Kipande namna ya kupandisha udongo kwenye mche wa muhindi wakati wa palizi wakati akikagua shamba la Mkuu wa Mkoa wa Katavi Desemba 18, 2012 eneo la tenki fupi kata ya Nsimbo, wilayani Mlele, Katavi. Bi. Kipande ni mfanyakazi katika shamba hilo.
 Waziri Mkuu Mizengo akipokea maelezo ya shamba kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Dk. Rajab Rutengwe (wa pili kulia) wakati alipoenda kukagua shamba la Mkuu huyo wa Mkoa Desemba 18, 2012 eneo la tenki fupi kata ya Nsimbo, wilayani Mlele, Katavi. Kulia ni Bi. Yusta Kipande na (kushoto) ni Bi. Grace Donald wanaofanya kazi kwenye shamba hilo .
Waziri Mkuu Mizengo akipokea maelezo ya shamba kutoka kwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi, Injinia Emmanuel Kalobelo (aliyenyoosha mkono) wakati alipoenda kukagua shamba lake Desemba 18, 2012 eneo la tenki fupi kata ya Nsimbo, wilayani Mlele, Katavi. (Picha na Irene Bwire wa Ofisi ya Waziri Mkuu).

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO