Monday 24 December 2012

Mahafari Ya 8 Ya SUZA Yafana

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ,akitoa zawadi kwa mwanafunzi bora katika fani ya Shahada ya Sanaa na Elimu, kwa Sabrina Saidi Rashid,katika sherehe za Mahafali ya nane ya Suza,huko katika kampasi ya Tunguu leo.
Baadhi ya Viongozi wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar walioalikwa katika sherehe za Mahafali ya nane ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) zilizofanyika leo katika kampasi ya Tunguu,Mkoa wa Kusini Unguja. .
Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ngazi ya Stashahada ya Lugha na Elimu, wakati walipokuwa wakitunukiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,(kulia) pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA), katika sherehe za mahafali ya nane ya Chuo hicho yaliyofanyika leo katika kampasi ya Tunguu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ,akitoa zawadi kwa mwanafunzi bora katika fani ya Cheti cha Teknolojia ya Habari,(IT) kwa Lukuman Mohamed Bachu,katika sherehe za Mahafali ya nane ya Suza,huko katika kampasi ya Tunguu leo. 
Baadhi ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,pia Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ,akitoa hutuba yake baada ya kuwatunuku Shahada,katika sherehe za Mahafali ya nane ya chuo zilizofanyika huko katika kampasi ya Tunguu
                     [Picha na Ramadhan Othman,Ikulu.]

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO