Wednesday 16 January 2013

AJALI MBAYA YATOKEA ASUBUHI YA LEO WILAYANI TUNDURU KATIKA ENEO MTAA WA MUUNGANO

Mkazi mmoja ambaye ni mkazi wa Tunduru na jina lake halikuweza kufahamika kwa haraka kutokana na sababu zisizo zuilika amepata ajali mbaya leo asubuhi wakati anatoka nyumbani kwake na kuelekea kazini kwake ambapo ni katika duka lake ambalon anauza madawa baridi lililopoa makabala na benki ya NMB Tawi la Tunduru.
 
Dereva huyo amejikuta akiingiza Gari katika korongo lililopo katika mtaa wa muungano karibu na ofisi za tanesco wilayani Tundru ambapo alikuwa anavuka daraja lililopo katika eneo hilo na hatimaye kushindwa na kujikuta anaingia katika bonde ivyo kujisababishia michubuko katika mwili wake na kwa sasa anaendelea vizuri.
 
Wakazi wa eneo hilo a muungano wamewahasa watumiaji wa vyombo vya moto kuwa makini pindi wanapoku wanaendesha ili kuepukana na ajali hizo

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO