Wednesday 16 January 2013

PAMOJA NA UJENZI WA BARABARA ITOKAYO MJINI SONGEA KUELEKEA WILAYANI TUNDURU KUFANYIWA UKARABATI LAKINI BADO BAADHI YA MAENEO NI BADOKERO KWA WASAFIRI.

Hii ndio hali halisi kwa barabar itokayo Songea kuelekea Tunduru katika maeneo ya kijiji cha Namingwea
Barabara ambayo inatokea Songea kuelekea Tunduru ambayo inafanyiwa ukarabati na makampuni mawlili tofauti ambayo ni Sogea Satom ambayo inadhamana ya utengenezaji wa barabara kuanzia Mjini Songea mpaka katika Wilaya ya Namtumbo ambayo inaonekana kuendelea vizuri na ukarabati huo na wapo katiaka hatuwa za mwisho za ukarabati huo.
Na kuanzia katika Wilaya ya Namtumbo mpaka wilayani Tunduru Kampuni ambayo inadhamana ya utengenezaji wa barabara hiyo ni Progressive ambayo inamilikiwa na wahindi,licha ya kampuni hiyo kusitishiwa mkataba wake wa ujenzi wa barabara hiyo lakini bado watumiaji wa barabara hiyo wapo katika wakati mgumu hasa katika kipindi hiki cha mvau.
haya ni baadhi ya magari ambayo yamenasa katika eneo hili
Magari mengi yakiwemo ya abiria na vilevile ya mizigo yameshindwa kuendelea na safari katika maeneo ya kijiji cha  Namingwea kilichopo wilayani Tunduru kutokana na halimbaya ya barabara na kusababisha magari hayo kukwema(kunasa)katika eneo hilo ivyo kusababisha abiria kushidwa kuendelea na safari zao na hata kukosa huduma muhimu kwani eneo hilo lipo polini sana na hivyo kuhatarisha maisha yao.
Aidha Mkuu wa wilaya ya Tunduru bwana Chande Nalicho alipo kuwa anatoka Mjini Songea kurudi na kurudi katika wilaya yake ya Tunduru naye pia alikumbana na tatizo hilo ambapo alinasa katika eneo hilo la kijiji cha Nmigwea zaidi ya mala tatu(3) na kulazimika kushika chepe na Jembe kwa ajiriya kufanya jitihada za kulitoa gari ambalo lilinasa katika tope zito ilikuendelea na safari na zoezi hilo lilichukuwa takribani saa nzima mpaka kufanikisha kupita katiak eneo hilo la Namingwea. 
Mkuu wa wilaya ya Tunduru wa kwanza kushoto na Mkurugenzi wa wilaya hiyo wa pili kutoka kulia wakiwa mzigoni
Wananchi wengi wamekuwa waathirika wakubwa kwani hakuna njia nyingine ya usafiri wanayoitegemea kutoka songea kuelekea Tunduru na kutoka tunduru kuekekea songea na wakaiomba serikali ilingalie kwa umakini zaid lakini pia Mkuu wa wilaya hiyo nae pia akiwa ni mmoja wa waathirika wa ubovu wa barabara hiyo pia aliiomba mamlaka husika  na ujenzi wa barabara hiyo iliangalie suala hilo kwa umakini mkubwa sana..

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO