Saturday 19 January 2013

MKUU WA WILAYA YA TUNDURU AAGIZA VITANDA VIPELEKWE ARAKA KATIKA ZAHANATI YA KITANDA.


Akiwa ndani ya zahanati hiyo
Mkuu wa wilaya ya Tunduru Bwana Chande Nalicho hii leo alipokuwa katiaka ziara yake ya kutembelea baadhi ya maeneo ambayo serikali ilitoa ahadi ya ujenzi wa miradi mbalimbali.

Mkuu huyo wa Wilaya ametembelea katiaka zahanati iliyopo katika kijiji cha Kitanda kata ya Mlingoti Mashariki wilayani Tunduru nakumuagiza Muuguzi mkuu wa wilaya ya Tunduru Bwana Norbet Haule kupeleka vitanda haraka iwezekanavyo katika Zahanati hiyo.

Agizo hilo amelitoa baada ya kukuta Zahanati haina kitanda hata kimoja.
Hivyo imepelekea kwa mama wajawazito ambao wanafika katika Zahanati hiyo kujifungua kwa shida na kuwaladhimu kulala chini .

Akiendelea kuzungumza Bw. Chande Nalicho amedai hakupendezwa na uongozi huo wa Zahanati kwa kuwalaza wagonjwa chini pale wanapokuja kupata tiba.

Katika taharifa fupi iliyosomwa na Muuguzi Mkuu wa wilaya ambapo amesema Ujenzi wa Zahanati hiyo umeghalim jumla ya 330,009,00/=(milioni mia tatu therathini na mia tisa) imejegwa  na TASAFU na katika ujenzi huo Serikali imechangia milioni sita/(6,000000/=) na Zahanati hiyo Bado inakabiliwa na tatizo kubwa la wauguzi(watumishi)ambapo mpaka sasa inajumla ya wauguzi(watumishi)wawili,tu na mmoja kati ya hao ni Elizabeth Mbepela.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO