Tuesday 29 January 2013

ZAO LA KOROSHO BADO NI GUMZO WILAYANI TUNDURU

WAKATI kukiwa na Sinto fahamu juu ya upatikanaji wa Soko la Uhakika la
kuuzia Korosho Wakulima wa zao hilo  wilaya Tunduru mkoani
Ruvuma,wameiomba serikali itoe kibali cha kuruhusu korosho zao kuuzwa
kwa wafanyabiashara binafsi ili kuwaepusha na hasara wanayoendelea
kuipata wakati  huu ambapo wanasubiri malipo yao ya mwaka uliopita.

Kilio hicho kumepazwa katika nyakati tofauti na wakulima hao na
kuungwa Mkono na Viongozi walioshiriki katika Mkutano Mkuu wa Dhalula
wa Chama kikuu cha Ushirika cha Wilaya ya Tunduru (TAMCU) kilicho keti
katika ukumbi wa Chama hicho

 

Wakifafanua taarifa hiyo wakulima hao walisema kuwa hali hiyo
inatokana na  muda wa uvumilivu kupita na hata kuvuka kikomo hivyo
wameamua kuchukua maauzi hayo ya kuitaka serikali ichukue hatua haraka
ili wasiendelee kupata hasara kama ilivyotokea katika msimu wa mwaka
2010/2011.

Walisema katika msimu huu zaidi ya tani 500 ya zao ilo hazikununuliwa
hali mabayo iliwasababishia hasara na matatizo mengi wakulima hao
ambao kwa sasa  wakulima hao hawataki kusikia tena neno la ushirika
kwani unawasababishia umasikini na kukubali kuuza mazao yao ikiwemo la
korosho kwa walanguzi wanaonunua kwa bei ndogo kuliko kusubiri bei ya
serikali ambayo haina uhakika.

 
Akizungumzia hali ya Mkanganyiko huo Meneja wa Chama Kikuu cha
Ushirika cha wakulima wa Tunduru (TAMCU) Bw. Imani kalembo alidai kuwa
hali hiyo inatokana na Chama hicho kukosa sifa za Kukopesheka baada ya
kushindwa kurejesha Deni la zaidi ya shilingi Bilioni.2.8 kati ya
fedha zilizokopwa msimu uliopita.

Alisemsa deni hilo lilishindwa kulipika kufutia ubabaishaji wa
wanunuzi wakubwa ambao alitelemsha bei kwa kiasi kikubwa na kukifanya
chama chao kuuza Korosho zao kwa Bei ya Tsh.850 kwa kilo moja kutoka
Tsh. 1200 walizonunulia kutoka kwa wakulima na kusabishiwa hasara hiyo

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO