Thursday 17 January 2013

MTOTO HUYU ANAHITAJI MSAADA WA MATIBABU

 
Mtoto Simoni Mlope
 Kulia ni mama wa mtoto Simoni Mlope ambaye anasumbuliwa na ugonjwa wa tundu kwenye moyo na kulazimika kukatisha masomo yake ya shule ya msingi. Hapo yupo nyambani kwake maeneo ya mahenge alipotembelewa na waandishi wa habari wa mkoa wa Ruvuma.
*************


Mtoto simon Mlope mwenye umri wa miaka 11 mkazi wa eneo la mahenge katika manispaa ya songea mkoani Ruvuma amelazimika kukatisha masomo yake ya shule ya msingi akiwa darasa kwanza  kutokana na mototo huyo kusumbuliwa na ugonjwa wa moyo .



Mtoto simon Mlope alikubwa na ugonjwa moyo  tangu mwaka 2001 mara baada ya kuzaliwa na kugundulika kuwa  moyo wake una tundu hali ambayo inasababisha  kuvuta pumzi kwa shida.



Mama wa mototo  simon mlope anayeitwa AMINA ALLY  anawaomba watanzania kumsaidia mtoto  wake fedha za matibabu Baada ya kuambiwa na madaktari kuwa simon anatakiwa kwenda nchini  india kutibiwa,baada ya kupata rufaa kutoka muhimbili mwaka 2006  huku familia yake ikiwa haina uwezo kabisa.



Majirani wa familia ya simon nao wanasema kuwa mototo simon anahitaji msaada wa haraka kwa kuwa hali yake sio nzuri na kuwaomba watanzania wamsaidie.



Kinachosikitisha zaidi baba wa mtoto huyo  anayejulikana kwa jina la SIMON MLOPE  ameondoka nyumbani hapo tangu mwaka 2011 na hajulikani aliko kwa sasa, ingawa mwanzoni alisema yuko nchini Msumbiji.

Kwa anayeguswa na tatizo hili na anataka kumsaidia  SIMONI MLOPE  atumie simu namba  0752732290

 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO