Monday 24 June 2013


  24.6.2013   SONGEA

Watuwannewakaziwakijiji cha Majala kata 
ya NandembowilayayaTunduru mkoani Ruvuma  wanatafutwa na jeshi la polisi kwatuhuma za kuyatelekeza meno kumi  na nane ya tembo wakati wakiyasafirisha kutoka kijiji cha ligunga kuelekea kijiji cha Majala.


Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wapolisi wa mkoa wa Ruvuma bwana DEUSDEDITI NSIMEKI amesema watuhumiwa haowalikimbia nakutelekeza baiskeli zao walipoona mwanga wataa  za gari likiwa na askari polisi.



Kamanda Nsimeki amesema watu hao walikuwa wamebeba pembe za tembo kumi na nane zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia mbili. Na mpaka sasa hakuna aliyekamatwa lakini polisi bado wanaendelea na msako mkali.

1.

Aidha kamanda Nsimeki ametumia nafasi hii kuwaomba wananchi Waendelee kuwaunga mkono polisi kwakuwapa ushirikiano wakutoa taarifa sahihi kama hii ambayo imewawezesha kukamata meno mengi ya tembo.


Akiwageukia waalifu ametoa onyo kali kwa kuwataka waache mara moja kuhu jumuu chumi wa nchi kwa kuwa vita ya kupambambana na wawindaji na wafanyabiashara wa meno ya tembo au raslimali nyingine za taifa haina suruhu kwa kuwa polisi namaliasili wamejipanga kuhakikisha tatizo hili linakwisha kabisa.


Hili ni tukio la tano kutokea la kukamata meno ya tembo katika mkoa wa Ruvuma ambapo uchunguzi wa awali haujaonyesha kama tembo wanaouwawa wanatokea katikaMbuga za selou au nchi jiraniyaMsumbiji.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO