Sunday 2 June 2013

WIKI YA MAZIWA YAMALIZIKA SONGEA DOKTA EMANUEL NCHIMBI AFUNGA MAADHIMISHO HAYO



Maadhimisho ya 17 ya wiki ya maziwa nchini yamefungwa leo mjini SONGEA mkoani RUVUMA kwa kutolewa matumaini na Serikali kuimalisha vituo vyake vya uhamilishaji wa ng’ombe wa maziwa vilivyopo mkaoni ARUSHA, MWANZA na MBEYA ili kusambaza kwa wafugaji ng’ombe wa kisasa kuongeza tija katika uzalishaji wa maziwa

Waziri wa mambo ya ndani ya nchi DAKTA EMMANUEL NCHIMBI akifunga maadhimisho ya wiki ya maziwa kwa niaba ya waziri wa mifugo na uvuvi DAKTA MATHAYO DAVID, amesema serikali inalitambua tatizo la upungufu wa ng’ombe wa maziwa na imeviimarisha vituo hivyo vya kanda vitakavyohudumia  pia katika mikoa ya jirani

Naye KAIMU MSAJILI wa bodi ya maziwa nchini DAKTA MAYASA SIMBA amesema maadhimisho ya mwaka huu yaamefana ukilinganisha na miaka mingine kutokana na wanafunzi wa shule za msingi na sekondari pamoja na wananchi wa kawaida kujitokeza kwa wingi

Wiki ya maziwa hapa SONGEA iliambatana na maonyesho ya bidhaa za maziwa zilizosindikwa ambapo kampuni ya ASASI DAIRIES ya IRINGA imejinyakulia ushindi wa jumla na meneja mauzo wa nyanda za juu kusini wa kampuni hiyo JIMMY KIWELU amesema vionjo mbalimbali walivyoweka kwenye bidhaa zao ndio zimevutia wateja wengi

Wadau wa baraza la maziwa wameadhimia kutekeleza program ya unywaji maziwa mashuleni na wamekubaliana maadhimisho ya mwaka kesho kufanyika mkoa wa MARA

Catherine Nyoni -RUVUMA    

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO