Thursday 30 May 2013

Kampuni ya usambazaji mbegu ya PANNAR SEED kanada ya kusini yatoa jezi 28 na mipira 5 kwa Timu za vijijini Songea


Meneja wa kanda ya kusini Torio Mafie toka kushoto kwako akiwa ameshikilia mpira pamoja na jezi wakati akimuonyesha mkuu wa wilaya ya Songea jana ofini kwake.
............................................
Hii ni baaada ya kukamilika kwa msimu wa mavuno kwa wakulima wa wilaya ya SONGEA mkoani RUVUMA sasa kampuni ya usambazaji mbegu ya PANNAR SEED kanda ya nyanda za juu kusini imetoa vifaa vya michezo wa soka kwa wakulima ili kufufua michezo wakati wakiwa waanajiandaa kwa msimu mwingine wa kilimo.

Kampuni ya PANNAR SEED imetoa jezi 28 na mipira mitano vyenye thamani ya shilingi milioni 2 na laki moja ambapo MENEJA WA KANDA YA KUSINI TORIO MAFIE amesema msaada huo waliotoa ni ishara kuwa wapo pamoja na wakulima ili kuwapa vijana shughuli mbadala wakati wa mapumziko ya msimu wa kilimo
Mkuu wa wilaya ya SONGEA JOSEPH MKIRIKITI Akipokea  jezi na mipira kutoka kwa wawakilishi wa kampuni ya
PANNAR SEED
Mkuu wa wilaya ya SONGEA JOSEPH MKIRIKITI akitabasamu kwa furaha baada ya wakulima kuwezeshwa vifaa vya michezo ,
 Hataa hivyo kwa mujibu wa mkuu wa wilaya ya SONGEA amesema bado mahitaji ya vifaa vya michezo ni makubwa hivyo ameziomba kampuni mbalimbali zinazojihusisha na shughuli za kiuchumi na kijamii wajitokeze kufadhiri timu za vijiji wilayani hapa

 

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO