Wednesday 22 May 2013

NILIYEKUTANA NAYE

                                                    ESTER HAULE( MRS MTEGA)

Cathy habari imekutana na mwanadada makini sana katika anga za ujasiliamali ambaye anafaa kuigwa na wanawake wengine. Ester ni mfanyakazi katika sekta ya afya kitengo cha utoaji dawa. ni mke wa mwandishi wa habari Nathani Mtega. Pamoja na kuwa mfanyakazi katika duka la dawa muhimu lakini yeye binafsi anajishugulisha na biashara ya uuzaji wa dawa katika duka lake mwenyewe lililopo katika eneo la msamala.Mpaka sasa amefanikiwa kujenga nyumba nzuri katika eneo la msamala anakoishi na malengo yake ni mengi ikiwemo kuendelea na kazi yake pamoja na kuendeleza duka la mume wake lililopo katika kata ya mjimwema songea ambalo nalo analisimamia na kuhakikisha linasonga mbele. Sifa nyingine ya Ester ni mcheshi, mkarimu na anapenda sana kupika.Ester ni mkazi wa Songea mkoani Ruvuma, Mungu akujalie ufanikiwe malengo yako.

No comments:

Post a Comment

TUPE MAONI YAKO